Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Brexit: Uingereza yakubali kuondoka kwa awamu
Baada ya siku ya kwanza na mazungumzo, mjini Brussels Ubelgiji, Uingereza imekubali mpango wa Muungano wa Ulaya wa kujiondoa kutoka kwa muungano huo kwa hatua.
Waziri wa Uingereza anayeongoza mpango huo David Davis, amekubali kusitisha mazungumzo kuhusu mikataba ya kibiashara kati ya pande hizo mbili hadi hatma ya raia wa pande hizo walioko mataifa ya EU na fidia ya mwisho ya utengano kuafikiwa.
Aidha amesema ni wazi kwamba pande zote mbili zinataka kupata kustakabali mzuri wa uhusiano wao.
Naye Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya katika mazungumzo hayo Michel Barnier amesema kwa pande zote mbili Umoja wa Ulaya na Uingereza makubaliano ya haki yanawezekana na ni bora zaidi kuliko kutofanya kabisa.