Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
FBI wamchunguza mkwe wa Trump, Kushner
Vyombo vya habari nchini Marekani vimeripoti kuwa Mkwe wa Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye pia ni mshauri wake mwandamizi Jared Kushner anachunguzwa na Shirika la upelelezi nchini humo FBI, juu ya tuhuma za Urusi kuingilia kati uchaguzi wa nchi hiyo mwaka uliopita.
Habari zinasema wachunguzi wanaamini kuwa Kushner anaweza kuwa na taarifa za uhakika kuhusiana na uchunguzi wao, lakini hatua hiyo sio lazima kumfanya kuwa yeye ni mshukiwa wa uhalifu.
Kushner anafahamika pia kwamba mwaka uliopita alikutana na balozi wa Urusi Sergei Kslyak pamoja na Mwenyekiti wa bodi, benki ya Urusi Sergei Gorkov.
Hata hivyo mwanasheria wake anasema mteja wake tayari alijitolea kuzungumza na bunge la Congress juu ya nini anachojua kuhusiana na mikutano hiyo yote ya viongozi hao.