Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maharamia wanadai fedha kuachia Meli, Somalia
Kikosi cha Jeshi la majini la kupambana na Uharamia la Umoja wa Ulaya, kimethibitisha kuwa watu wenye silaha wanataka kupewa fedha, kuiachia meli ya mafuta iliyokamatwa nje kidogo ya pwani ya Somalia siku ya Jumatatu.
Kikosi hicho kimesema kimefanya mawasiliano kwa njia ya simu na mmiliki wa meli hiyo, ambaye amesema meli na wafanyakazi wake walikamatiwa Kaskazini mwa pwani ya Puntland.
ARIS-13 ilikuwa ikisafiri kutoka Djibouti kwenda katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu wakati ilipotuma alama ya hatari ikisema kuwa inafuatwa na boti inayokwenda kasi.
Hii ni mara ya kwanza kwa meli ya kibiashara kutekwa nyara baharini katika eneo la pwani ya Somalia tangu mwaka 2012.
Maharamia walikuwa wamepiga kambi katika maeneo hayo mpaka pale vikosi vya jeshi la majini vya Umoja wa Ulaya vilipoanza kufanya doria na kudhibiti hali hiyo.