Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wasichana 2 washambuliaji wa kujitolea mhanga wauawa Nigeria
Polisi nchini Nigeria wanasema kuwa wasichana wawili wanaokisiwa kuwa washambuliaji wa kujitoa mhanga, wameuawa kwa kupigwa risasi wakati walijaribu kuingia kaskazini mashariki mwa mji wa Maiduguri saa za usiku.
Polisi walisema kuwa kikosi cha kupambana na wanamgambo wa jihad kiliwafyatulia risasi wasichana hao wenye umri wa miaka 18 kabla ya kulipua milipuko yao.
Milipuko hiyo kisha iliharibiwa kwa nji salama.
Kundi la Boko Haram ambalo lilianzia mjini Maiduguri, limekuwa likiwatumia wanawake kama washambuliaji wa kujitoa mhanga.