Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Hospitali zaanza kuwafuta kazi madaktari Kenya
Hospitali nchini Kenya zimeanza kuwafuta kazi madaktari wanaogoma na kuwaondoa kutoka wa nyumba zao.
Huduma kwenye hospitali za umma zimetatizika kutokana mgomo ambao ulianza mwezi Disemba, huku madaktari na wahudumu wengine wa afya wakitaka mshahara zaidi na mazingira bora ya kufanya kazi.
Lakini hatua hiyo ya kuwafuta kazi madaktari inakuja wakati chama cha madaktari kinasema kuwa kimetia sahihi nyaraka zinazohitajika ili kumaliza mgomo wao.
Madaktari nao wanaitaka serikai kufanya hivyo.
Lakini serikali inasema kuwa siku ya mwisho ya kukubali asilimia 50 ya nyongeza ya mshahara ilipita siku mbili zilizopita.
Sasa hospitali zimeanza kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya madaktari ambao wamekuwa kwenye mgomo kwa siku 95.