Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kenya: Mahakama yatoa makataa kwa madaktari waliogoma
Madaktari sita kutoka muungano wa madaktari nchini Kenya wamepewa muda wa wiki mbili kumaliza mgomo wao la sivyo wafungwe jela wiki mbili.
Mgomo huo ambao umeendelea kwa zaidi ya mwezi mmoja umeathiri pakubwa shughuli za matibabu katika hospitali za umma.
Mahakama ya Ajira na mahusiano ya kazi nchini Kenya imeamuru muungano wa madaktari kusitisha mgomo huo na kumaliza mazungumzo na serikali katika kipindi cha wiki mbili zijazo.
Juhudi kadhaa za kumaliza mgomo huo zimegonga mwamba huku madaktari wakitaka kutekelezwa kikamilifu kwa mkataba uliosainiwa baina yao na serikali mwaka 2013 ili kuboreshwa kwa malipo na hali bora za kazi.
Jaji Hellen Wasilwa amesema kuwa iwapo maafisa watakaidi amri ya mahakama watafungwa jela wiki mbili.