Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ibrahimovic apigwa marufuku mechi tatu
Mshambuliaji wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic, amapigwa marufu ya mechi tatu, baada ya kumchezea vibaya mchezaji wa Bournemouth Tyrone Mings, walipotoka sare ya 1-1 siku ya Jumamosi.
Hii inafuatia kisa kilichotoea mnamo dakika ya 44. Kisa hicho hakikutambuliwa na maafisa wa mechi lakini kilinaswa kwenye video.
Mfungaji huyu bora wa Manchester, sasa atakosa mechi kati ya Man U na Chelsea na pia Middlesbrough na West Brom.
Hata hivyo atacheza mechi ya nyumbani na Everton tarehe 4 mwezi Aprili.