Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Asema alilazimishwa kukiri kumuua Kim Jong nam na Malaysia
Mtu mmoja anayeshukiwa kuhusika na mauji ya ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, amesema kuwa yeye ni mhanga wa hujuma za utawala wa Malaysia dhidi ya Korea Kaskazini.
Akizungumza mjini Beijing baada ya kuwasili kutoka Malaysia, Ri Jong Chol, amelaumu polisi wa Malaysia, kwa kutishia familia yake, iwapo hatakiri kuhusika kwake na mauaji ya Kim Jong Nam.
Hapo jana Ijumaa maafisa nchini Malaysia walisema, wana ushahidi wa kutosha, kumfungulia mashtaka Bw. Ri, na kwamba atarejeshwa kwao kwa kosa la kukiuka sheria ya uhamiaji ya nchi hiyo.