Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu wenye vipara washerehekea Japan
Zaidi ya wanaume 30 wenye vipara kichwani nchini Japan wanaadhimisha siku kuu yao ya kila mwaka inayoshirikisha mchezo wa kuvuta kamba.
Klabu hiyo ya wenye vipara inawajumuisha wananchama 65 kutoka maeneo tofauti nchini tangu ibuniwe 1989.
Lengo ni kuwahamasisha watu zaidi kuhusu watu wenye vipara
Mwenyekiti wa klabu hiyo Teijiro Sugo mwenye umri wa miaka 70 alisema kuwa matumaini ni kwamba klabu hiyo ingewavutia wanachama zaidi na kuwa kubwa zaidi.
''Nawataka wanaume wote walio na upara duniani kukongamana hapa ili kuanzisha michezo ya olimpiki'',alisema.