Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
DR Congo: Tshisekedi asafirishwa Ubelgiji kwa matibabu
Kiongozi wa upinzani nchini DR Congo Etienne Tshisekedi ameelekea nchini Ubelgiji kwa matibabu ya kiafya kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Chombo hicho cha habari kimeongezea kuwa hatua hiyo inajiri wakati ambapo chama chake kinaendelea na mazungumzo ya kugawana mamlaka kufuatia hatua ya rais Laurent Kabila kukataa kujiuzulu baada ya muda wake wa kuhudumu kukamilika mwezi uliopita.
Viongozi wa kanisa la Katoliki nchini humo walifanikiwa kuweka makubaliano ambapo bwana Tshisekedi alitarajiwa kupewa wadhfa wa serikali ya mpito hadi pale uchaguzi utakapofanyika mwishoni mwa mwaka huu.