Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Iran: Mkataba wa nuklia hautajadiliwa tena
Mpatanishi mkuu wa mpango wa nukilia wa Iran na mataiafa makubwa duniani, amesema kuwa mapatano yaliyoafikiwa hayatajadiliwa tena wakati rais mteule wa Marekani anajiandaa kuingia madarakani.
Abbas Araghchi ambqye pia ni waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Iran, alirejelea matamshi ya onyo kutoka kwa kiongozi mkuu nchini Iran Ayatollah Ali Khamenei, ambapo alisema kuwa watachoma mkataba huo ikiwa utavurugwa.
Trump ametaja makubaliano hayo ya kupunguza shughuli za kinyukila za Iran uliofakiwa mwaka mmoja uliopita kama mabaya zaidi kuwai kuafikiwa.