Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maprofesa waliotekwa na Taliban waoneshwa kwenye video
Wapiganaji wa Taliban wametoa kanda ya video inayowaonesha mateka wawili - Mmarekani na raia wa Australia - ambao walitekwa na wanamgambo hao nchini Afghanistan mwaka jana.
Mmarekani Kevin King na raia wa Australia Timothy Weekes walikuwa maprofesa katika chuo kikuu cha Wamarekani cha Afghanistan mjini Kabul.
Walitekwa mwezi Agosti wakiwa kwenye magari yao nje ya chuo hicho na wapiganaji waliokuwa wamevalia sare za wanajeshi wa serikali.
Baadaye mwezi huo, wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan walijaribu kuwakomboa lakini wakashindwa, Pentagon ilisema.
Kwenye video hiyo ambayo inadaiwa kupigwa mnamo 1 Januari na kupakiwa mtandaoni, wanaume hao wanasema wamo buheri wa afya.
Lakini wanamuomba Rais mteule wa Marekani Donald Trump kujitolea kuwabadilisha na wafungwa wa Taliban ndipo waachiliwe huru.
Wanasema watauawa iwapo Marekani haitashiriki kwenye mazungumzo ya kuwaachilia huru.