Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Caster Semenya afunga pingu za maisha
Mshindi wa nishani ya dhahabu katika mashindano ya olimpiki raia wa Afrika Kusini Caster Semenya amefunga ndoa na mpenzi wake mwishoni mwa wiki.
Bingwa huyo wa mbio za akina dada za mita 800 ambaye amekuwa akikumbwa na mzozo kuhusi jinsia yake, alimuoa Violet Raseboya aliyevalia gauni nyeupe.
Semenya alitaja harusi kuwa siku muhimu kwao na kusambaza picha zake kwenye mitandao ya kijamii.