Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Muuaji wa watu 39 katika kilabu ya burudani Uturuki asakwa
Maafisa wa polisi nchini Uturuki wanamsaka mshambuliaji aliyewafyatulia risasi watu waliokuwa wakisherehekea kuingia kwa mwaka mpya katika klabu moja ya burundani mjini Istanbul.
Waziri wa maswala ya ndani nchini Uturuki Suleyman Soylu anasema kuwa watu 39 wamefariki ikiwemo raia 15 wa kigeni huku zaidi ya watu 70 wakipelekwa hospitali na majareha .
Waziri huyo amekana madai kwamba kulikuwa na zaidi ya mtu mmoja aliyekuwa akiwafyatulia watu risasi kiholela.
Rais wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan amesema kuwa mashambulio kama hayo yanalenga kuliyumbisha taifa na amewataka raia wa Uturuki kuungano dhidi ya kile lichokitaja kuwa ''mchezo mchafu''.