Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump aitaka Israel kusitisha ujenzi katika ardhi ya Palestina
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amelitaka azimio la baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kusitisha ujenzi wa makaazi ya Israel katika ardhi ya Palestina.
Katika taarifa iliotolewa kabla ya kura hiyo inayotarajiwa baadaye siku ya Alhamisi, Bw Trump amesema kuwa amani haitaafikiwa kupitia hatua ya Umoja wa Mataifa kuweka masharti.
Azimio hilo litaagiza kwamba shughuli zote za makaazi hayo katika eneo hilo la Palestina, ikiwemo Jerusalem mashariki lazima zisitishwe.
Marekani imekuwa ikiunga mkono Israel katika Umoja wa Mataifa, lakini wanaounga mkono azimio hilo wamekuwa wakitumai kwamba utawala wa rais Obama utasusia kura hiyo.