Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Al-Qaeda yathibitisha kuuawa kwa kiongozi wao
Kundi la kigaidi la Al-Qaeda limethibitisha kuuawa kwa kiongozi wao mkubwa Farouq al-Qahtani huko kaskazini Mashariki mwa Afghanistan katika mapigano na vikosi vya marekani mwezi mmoja uliopita.
Huko mjini Washington wamethibitisha kifo hicho kutokea November 15 yalikuwa ni makabiliano adhimu.
Lakini Al-Qaeda wamesema kuwa mkewe na watoto waliuwawa pia japo hawakujulikana kijeshi.
Vikosi vya Marekani vimeiweka Al-Qahtani mzaliwa wa Saudi huko Quatar kama mtu wanayemtafuta sana kwao akituhumiwa kuhusika na mipango ya mashambulizi huko Marekani na Ulaya.