Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Magufuli atia saini sheria ya wanahabari
Rais wa wa Tanzania John Pombe Magufuli ametia saini Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 ambayo imekuwa ikipingwa na wadau katika sekta ya uanahabari nchini humo.
Sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge la Tanzania Jumamosi 5 Novemba mjini Dodoma.
Taarifa kutoka kurugenzi ya mawasiliano ya rais imesema Rais Magufuli alitia saini Sheria hiyo tarehe 16 Novemba na kwamba anaamini sheria hiyo itakuwa na manufaa mengi.
"Naamini kuwa Sheria hii itasaidia kuboresha sekta ya habari kwa manufaa ya wanataaluma wenyewe na Taifa," amesema Rais Magufuli.