Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wapinzani waandamana Zimbabwe
Polisi wa kutuliza ghasia nchini Zimbabwe wamerusha mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji wa upinzani katikati ya mji wa Zvishavane.
Chama cha Movement for Democratic Change kimetoa malalamiko kwamba polisi wamewatia mbaroni wafuasi wake licha ya amri ya mahakama kuruhusu maandamano hayo kuendelea.
Kumekua na maandamano katika miezi ya hivi karibuni nchini humo dhidi ya serikali ya Rais Robert Mugabe kutokana na kudorora kwa uchumi na kuanzishwa kwa mipango ya noti mpya.