Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kiongozi wa Iran adharau mwenendo wa kampeni za Marekani
Kiongozi mkuu wa Irani Ayatollah Ali Khamenei, amedharau mwenendo wa kampeni za urais Marekani.
Amesema kuwa matamshi ya wagombea wote wawili wakati wa midahalo yote ni ushahidi wa uvunjifu wa thamani ya binadamu nchini Marekani.
Ameonya kudhibiti siasa nchini Iran dhidi ya makubaliano ya moja kwa moja na Marekani kwa jambo lolote.
Katika hotuba tofauti Rais Hassan Rouhani ameelezea kuwa chaguo lililombele ya raia wa Marekani kuwa ni baya na chafu.
Na aliyekuwa Rais wan nchi hiyo Akbar Hashemi Rafsanjani amemuelezea Donald Trump kuwa ni mtu hatari.
Wairani wanaona kwamba kama Trump atashinda basi itakuwa ni vilio kuhusu makubaliano ya Nuklia na nchi zenye nguvu duniani, na kuanzishwa tena kwa vikwazo.