Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kiongozi wa IS auawa kwa shambulizi za ndege za angani Syria
Pentagon imethibitisha kuwa kiongozi wa kundi la kigaidi lenye itikadi kali la dola la kiislam Abu Mohamed al-Adnani ameuawa katika shambulizi la anga huko kaskazini mwa Syria mwezi uliopita.
Taarifa ya msemaji wake imeeleza kuwa ndege ya Marekani ilifanikiwa kumlenga na kumuua.
Kundi la dola la kiislam lilithibitisha kuwa amekufa, lakini Marekani na Urusi wote wanadai kuhusika na shambulio hilo.