Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Boko Haram wapigana wenyewe kwa wenyewe Nigeria
Wapiganaji wa kundi la Kiislamu la Boko Haram nchini Nigeria wamepigana wenyewe kwa wenyewe kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, duru za kiusalama zimeambia BBC.
Maelezo kuhusu mapigano hayo yaliyotokea katika eneo la Monguno, jimbo la Borno karibu na Ziwa Chad bado ni finyu kutokana na kutokuwepo kwa mawasiliano ya simu za mkononi maeneo hayo.
Mapigano yametokea baada ya kundi linalojiita Islamic State (IS) kutangaza mwezi uliopita kwamba Abu Musab al-Barnawi ndiye kiongozi mpya wa Boko Haram, na kumuondoa Abubakar Shekau.
Lakini Bw Shekau, ambaye awali alikuwa ametangaza kujiunga na IS, alisema bado anaongoza kundi hilo.
Baadhi ya wachanganuzi wanasema mgawanyiko katika kundi hilo huenda ukawafaa wanajeshi wa Nigeria katika juhudi zao za kukabiliana na wanamgambo hao.
Kufikia sasa, jeshi la Nigeria halijatamka lolote kuhusiana na mapigano hayo.