Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
China yaonya kuhusu uhuru wa Hong Kong
China imesema kwamba inaunga mkono hatua za kisheria dhidi ya yeyote anayetetea uhuru wa eneo la Hong Kong.
Onyo hili limejiri baada ya wanaharakati wanaounga mkono uhuru wa Hong Kong kushinda uchaguzi wa bunge.
Msemaji wa afisi ya China inayohusika na masuala ya Hong Kong na Macao amesema Beijing inapinga harakati zote za kutetea uhuru wa Hong Kong ndani na nje ya bunge
Raia wengi wa Hong Kong wameghadhabishwa na kile wanasema kuwa juhudi za China kuzima haki na uhuru wa kimsingi.