Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Matunda na mboga hupunguza hatari ya ugonjwa wa moyo
Utafiti mpya uliofanywa nchini Italy unasema kuwa chakula kinachotumiwa katika eneo la Mediterranean kinapunguza hatari ya vifo vya mapema miongoni mwa watu walio na ugonjwa wa moyo.
Utafiti huo umebaini kwamba watu wanaotumia matunda,mboga,samaki na njugu hupunguza hatari ya kufariki ikilinganishwa na wale wanaokula nyama nyekundu na siagi.
Mmiliki wa ripoti hiyo amesema kuwa mpango huo wa chakula unaweza kuwasaidia sana wagonjwa wa moyo ikilinganishwa na dawa zinazopunguza kiwango cha mafuta mwilini.
Tafiti za awali kuhusu umuhimu wa chakula hicho zimelenga kukinga visa vya ugonjwa wa moyo.