Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Polisi wakabiliana na waandamanaji wa Upinzani Zimbabwe
Polisi wamefyatua gesi za kutolea machozi na mabomba ya maji katika mji mkuu wa Zimbabwe Harare, kinyume na amri iliyotolewa na mahakama iliyowataka kutoingilia kati maandamano.
Makabiliano yalichacha pale waandamanaji walipoamua kujibu mashambulio ya polisi kwa kuwarushia mawe na kuchoma mataili ya magari.
Kiongozi wa upinzani Joice Mujuru amesema kuwa zaidi ya watu hamsini wamejeruhiwa.
Makundi ya upinzani yaliandaa maandamani kushinikiza mageuzi ya sheria ya uchaguzi kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2018.
Robert Mugabe --mwenye umri wa miaka 92 anasema anatarajia kugombea kiti hicho.
Kumekuwa na ongezeko la idadi ya maandamano ya upinzani dhidi ya serikali nchini Zimbabwe.