Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Barua pepe: Jaji amtaka Clinton kujibu mashtaka
Jaji mmoja wa Marekani amesema kuwa mgombea wa urais wa chama cha Democratic, Hillary Clinton lazima ajibu mashtaka yanayomkabili kuhusiana na matumizi mabaya ya barua pepe kwa maandishi kuelezea hali ilivyokuwa alipokuwa waziri wa maswala ya kigeni.
Kundi moja la wakereketwa wasiopendelea mabadiliko, Judicial Watch, limeishtaki wizara ya mashauri ya kigeni juu ya swala hilo likimtaka bi Clinton kutoa ushahidi binafsi chini ya kiapo.
Shirika la upelelezi la FBI lilikamilisha uchunguzi wake katika barua pepe hizo mwezi uliopita, bila kupendekeza mashtaka yo yote dhidi ya bi Clinton.