Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Aliyeokolewa kutoka Boko Haram asema anamkosa baba wa mtoto
Msichana mmoja raia wa Nigeria ambaye aliokolewa kutoka mikononi mwa kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram, amesema anamkosa sana mpiganaji wa kundi hilo ambaye ni baba wa mtoto wake.
Amina Ali ni mmoja wa wasichana mia mbili wa shule ya Chibok waliotekwa nyara miaka miwili iliyopita.
Amesema kile anachotaka sasa ni kwenda nyumbani.
Yeye pamoja na mtoto wake wamekuwa wakizuiliwa katika mjini Abuja, katika kile serikali inasema ni mpango wa kumwezesha kutengamana na watu tena.
Amina Ali alipatikana katika msitu mmoja mapema mwaka huu akiwa na mtoto wake na mtu mmoja ambaye alisema ni mumuwe ambaye ni mpiganaji wa kundi hilo la Boko Haram.