Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtaalamu wa nyota anayewachochea wasichana kupenda sayansi
Mtaalamu mmoja wa nyota nchini Kenya, anasafiri pamoja na darubini yake katika maeneo ya mashambani nchini humo, kwa lengo la kuwachochea watoto wasichana kuyapenda mambo yanayohusu sayansi.
Mradi huo wa Susan Murabana una lengo la kujenga kituoa cha kwanza cha umma cha kutazana nyota.
Ana matumani kuwa mradi huo utabuni ajira kwa wanafunzi wa masuala ya sayansi nchni Kenya, na pia kuwavutia watu kutoka eneo lote la Afrika ya Mashariki.
Anasema kuwa bado watu hawajaelewa jinsi sayansi ya nyota inaweza kutumiwa katika nyanja zingine maishani.