Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wahamiaji 21 wazikwa Libya
Wahamiaji 21 waliozama wameripotiwa kuzikwa na wakazi wa mji wa Libya baada ya miili yao kukutwa ikielea ufukweni.
Mamlaka nchini humo zinasema zililazimika kuchukua hatua ya kuondoa maiti zilizokuwa zinazagaa.
Miili hiyo ilikaa siku tatu katika pwani ya Al- Maya, kaskazini mwa Tripoli .
Wenyeji wa eneo hilo walijawa na hofu ya maiti hizo kusababisha magonjwa ndipo wakalazimika kuzizika.