Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Afrika Kusini: ANC yakabiliwa na ushindani mkali
Huku nusu ya kura zikiwa zimehesabiwa kwenye uchaguzi wa Afrika Kusini chama tawala cha African National Congress ANC kinakabaliwa na ushindani mkali zaidi tangu kiondoe utawala wa ubaguzi wa rangi mwaka 1994.
Tayari kimepata asilima 50 ya kura hizo hadi sasa huku mpinzani wake mkubwa chama cha Democtratic Alliance kikijipatia asilimia 34.
Katika uchaguzi wa Mabaraza miaka mitano iliyopita ANC ilishinda thuluthi mbili ya kura.
Ukosefu mkubwa wa ajira na sakata za ufisadi zinazomuandama rais Jacob Zuma na wengine umeathiri umaarufu wa chama hicho.