Malkia Elizabeth II: Wanandoa walifungua kadi kutoka kwa malkia siku aliokufa

Chanzo cha picha, RAY PONT
Wanandoa wamezungumza juu ya hisia zao tofauti kuhusu kufungua kadi iliyotiwa saini na Malkia Elizabeth II siku ambayo alikufa.
Tricia na Ray Pont kutoka Godalming, Surrey, walisherehekea kumbukumbu ya miaka 60 ya ndoa yao Alhamisi.
Wanandoa hao walifahamu kuhusu ugonjwa wa Malkia walipokuwa kwenye chakula cha mchana cha sherehe.
Wastaafu walisema ilikuwa "siku ya hisia mesto " ambayo "hawatasahau kamwe".
Wanandoa wote wanaofikia miaka 60 ya ndoa hupokea kadi ya pongezi kutoka kwa malkia.

Chanzo cha picha, RAY PONT
Bi Pont alisema: "Nilifurahi sana kufungua kadi. Nilidhani ungekuwa wakati mzuri sana kwa familia yetu.
"Inaifanya kadi hiyo kuwa ya thamani zaidi na ya kuhuzunisha kwani tulikuwa mmoja wa watu wa mwisho kupata mawasiliano kutoka kwake."
Bwana Pont alisema: "Sote wawili tulirudi nyumbani kutoka kwa chakula chetu cha mchana na tukatazama kadi na tukahisi machozi.
"Tulivunjika moyo kabisa na tukafadhaika sana."
Bi Pont alielezea jinsi kadi hiyo ilivyokuwa na picha ya Malkia mbele iliyopigwa kwenye roshani ya Kasri la Buckingham akisherehekea Jubilee yake ya Diamond mnamo Juni.
Alisema: "Ina maana sana. Ilikuwa na ujumbe mzuri ndani na ulitiwa saini kwa mkono."
Bi Pont, ambaye sasa ana umri wa miaka 80, alijieleza kuwa "mwanamfalme kamili" tangu alipokuwa mtoto.
Alielezea jinsi wazazi wake walimpeleka London mnamo 1947 usiku wa kabla ya harusi ya Malkia.
Alisema: "Tulisimama kwenye reli kwenye kasiri la Buckingham walipotoka kwenye roshani. Ilikuwa furaha."

Chanzo cha picha, RAY PONT
Bi Pont alisema baadaye alienda kwenye karamu ya bustani katika Kasri la Buckingham kwa niaba ya Chama cha Waelekezi wa Wasichana mbele ya Malkia, ambayo alielezea kama "heshima kubwa".
Alisema: "Malkia amekuwa sehemu ya ndani ya maisha yangu yote.
"Ninahisi bahati sana kuwa na mawasiliano na Ukuu wake."












