Nini kinaweza kutokea baada ya mauaji ya Qasem Soleiman?

fujo zinazoendelea baada ya mauaji ya Soleimani
Maelezo ya picha, Fujo zinazoendelea baada ya mauaji ya Soleimani

Kuuliwa kwa jenerali Qasem Soleimani, kiongozi wa kikosi maalum cha jeshi la ulinzi wa Iran nje ya nchi kinachofahamika kama Quds, kinachohusishwa katika mzozo wa kiwango cha chini kati ya Marekani na Iran, huenda matokeo yake lazimu kuwa na mwisho mbaya.

Kulipiza kisasi kutokana na mauaji hayo ni jambo ambalo linatarajiwa.

Mlolongo wa hatua za kulipiza kisasi kunaweza kuzifikisha nchi hizo mbili kufikia karibu katika mzozo wa moja kwa moja.

Siku za mbeleni, Marekani inaweza kutakiwa kuhojiwa na Iraq.

Na harakati za Rais Trump katika kanda hiyo-kama zipo zozote - zitafuatiliwa kwa karibu zaidi ya awali.

Philip Gordon, ambaye ni mratibu wa Ikulu ya Marekani na mataifa ya Uarabuni wakati wa utawala wa Obama, kuelezea mauaji hayo ni uhalalisho wa vita kati ya Wamarekani na Wairan.

mgogoro wa Marekani na Iran

Chanzo cha picha, EPA

Jeshi la Quds ni sehemu ya jeshi la usalama la Iran ambalo linafanya kazi katika mataifa ya kigeni.

Kwa miaka mingi Lebanon, Iraq, Syria au maeneo mengine, Soleimani alikuwa kiongozi mkuu katika kupanga mashambulizi au kuweka mikakati ya ulinzi katika maeneo yao.

Qassem Soleimani stands at the frontline during offensive operations against Islamic State militants in the town of Tal Ksaiba in Salahuddin province

Chanzo cha picha, Reuters

Kwa Marekani , alikuwa mwanaume ambaye alilengwa sana.

Lakini alikuwa maarufu Iran pekee. Na alihusika katika kuongoza mapigano na kampeni zilizokuwa zinaongozwa na mataifa ya nje pamoja na kupinga vikwazo ambavyo Marekani ilikuwa imeviweka.

Ni jambo gani ambalo lilishangaza sio kwamba Soleimani alianza hivi karibuni kupinga mambo ya rais Trump, lakini kwa nini Marekani wameamua kumuua sasa.

Maelezo ya video, Nini kinachoendelea kati ya Iran na Marekani

Mfululizo wa mashambulizi ya roketi dhidi ya Marekani ambayo Iran ilikuwa inalaumiwa Tehran. Mmoja wa mhandisi ambaye ni raia wa Marekani aliuliwa.

Ingawa awali operesheni ya Iran - mashambulizi yalikuwa dhidi ya Marekani katika eneo la mafuta lakini Marekani haikujibu kwa lolote.

Kulikuwa na mashambulizi ya anga vilevile na aliaminika kuwa nyuma ya operesheni hiyo. Tukio ambalo lilishambulia ubalozi wa Marekani huko Baghdad.

Katika kuelezea uamuzi wa kumuua Soleimani, Pentagon haijalazimika tu kuangalia matukio ya nyuma lakini pia mashambulizi ambayo yalimaanisha kuzuia uhalifu.

Kiongozi wa Pentagon ametoa tamko na kusema kuwa "mipango imepangwa kuwashambulia wanadiplomasia wa Marekani na watumishi wengine waliopo Iraq na katika ukanda wote".

Kinachofuata baada ya hapo ni swali kubwa.

RaisTrump ana matumaini kuwa tukio moja kubwa basi ndio litamuwezesha kuithibiti Iran na washirika wake kama Israel na Saudi Arabia wanahisi kuwa na nguvu bado.

Hata hivyo haijadhaniwa kuwa kutatokea muitikio wa haraka kutoka kwa Wa-Irani.

Inawezekana kuwa Iran ikawashambulia askari wa Marekani waliopo Iraq ili kulipiza kisasi?

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Inawezekana kuwa Iran ikawashambulia askari wa Marekani waliopo Iraq ili kulipiza kisasi?

Vikosi 5000 vilivyopo Iraq ndio vinaweza kulengwa zaidi. Hofu itakuwa kubwa katika mataifa hayo

Ingawa matokeo yataathiri bei ya mafuta.

Marekani na washirika wake wanaangalia namna ya kujilinda.

Marekani tayari imeimarisha ulinzi katika ubalozi wake. Kuna mipango ya kuongeza ulinzi haraka iwezekanavyo kama utahitajika.

Lakini pia kuna uwezekano kuwa kuna mzozo kwa majibizano ya maneno.

Mpambano dhidi ya jeshi la Quds lilikuwa wazi kwa jeshi la intelijensia ya Marekani.

Lakini je kumuua kiongozi huyo lilikuwa jambo la busara kufanya?

Je, Iran wanaweza kuwa wavumilivu kutotaka kulipiza kisasi?