Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
China yaonyesha uwezo wake wa kijeshi kwa gwaride la nguvu
Mamilioni ya watu nchini China na maeneo mengine duniani yameangalia mubashara gwaride la maadhimisho ya miaka 70 ya nchi hiyo kupitia televisheni na mtandaoni.
Televisheni ya taifa ya nchini humo ya CCTV ilianza matangazo hayo kwa kauli mbiu ya kuwatakia maisha marefu raia wa taifa hilo.
Maadhimisho hayo ya aina yake zimepambwa na gwaride la kijeshi la askari wapatao 188 .
Wanatarajia pia kurusha ndege 150 hii leo na tayari nyingine zimeanza kurushwa.
Wananchi wanafuatilia kwa karibu maadhimisho hayo huku wakijipiga picha za ukumbusho wa siku hiyo muhimu katika historia ya nchi yao.
Silaha mpya za DF-41 ambazo wachambuzi wanasema kuwa zimelengwa kutumika sehemu yoyote ulimwenguni.
Ulinzi mkali umetawala wakati wa shughuli hizi zikiendelea katika mitaa mbalimbali.
China ikiwa na sababu kubwa na nzuri ya kusheherekea siku hii baada ya kupita hatua ya kuwa taifa maskini na sasa ni taifa la pili duniani kwa kuwa na uchumi mkubwa duniani.