Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kijana mwenye miaka 17 aliyejitengenezea simu
Kijana wa miaka 17 kutoka nchini Canada ambaye alijitengenezea mwenyewe simu baada ya mama yake mSomali kusema kuwa hana uwezo wa kumnunulia simu ya smartphone amezungumza na BBC.
Mo Omer - ambaye anajiita mwenyewe "tech nerd" - alitengeneza simu ya smartphone kuanzia mwanzo , na anasema ataiuza kwa dola $180.
"Ina kila kitu unachoweza kukipata katika simu ya kawaida, ni kwamba tu haina gharama kubwa ," ameiambia BBC.
Simu "sio vifaa vigumu kutengeneza", aliongeza- na akasema ana azma ya kuzipeleka katika baadhi ya maeneo ya Afrika.
"Tumepokea maombi kutoka Nigeria na Algeria na maeneo mengine mengi. Ni soko linalokua kwa kasi ambalo tungependa kuingia ".