Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
UEFA: Ajax yaifumua Lyon katika Europa Ligi
Klabu ya soka ya Ajax ya Uholanzi imefanikiwa kuichapa Lyon ya Ufaransa bao 4-1 katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya michuano ya Uefa Europa mchezo uliopigwa dimba la Amsterdam Arena.
Magoli ya Ajax yamefungwa na wachezaji Bertrand Traore mabao mawili, Kasper Dolberg, Amin Younes na huku bao la kufutia machozi la Lyon likifungwa na Mathieu Valbuena.
Mchezo wa kwanza mwingine wa Nusu fainali unapigwa leo Alhamisi ambapo Manchester United watakuwa ugenini dhidi ya Celta vigo vijana wa Eduardo Berizzo,na wakati huo huo imeripotiwa ya kwamba wachezaji waliokuwa wanakabiliwa na majeruhi wanne wa Manchester United Paul Pogba, Eric Bailly, Chris Smalling na Phil Jones watakuwepo katika mchezo huo.