Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mimi ni mjamzito:Serena
Mchezaji wa tenisi nambari mbili kwa sasa duniani, Serena Williams amejitokeza katika mitandao ya kijamii na kuandika kuwa ni mjamzito.
Mwanadada huyo mwenye mika 35 aliweka picha yake kwenye snapchat akiwa amejipiga picha kwenye kioo na kuandika 20 weeks yaani majuma 20 kisha akaifuta hiyo post.
Iwapo itathibitika kwa hakika kuwa ni mjamzito, Serena anaweza kuzikosa Grans Slams tatu yaani French Open, Wimbledon na US Open.