Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanamgambo wawatoa jela wenzao Ufilipino
Wanamgambo nchini Ufilipino waliotangaza kulitii kundi la Islamic State wamewafungulia kutoka jela wapiganaji wenzao wanane wakati wa uvamizi uliofanywa kwenye gereza moja katika mji ulio kusini mwa Marawi.
Polisi wanasema kuwa takriban wapiganaji 20 kutoka kundi la Maute walivamia gereza la Lanao del Sur Jumamosi usiku na kuwapokonya silaha walinzi.
Wanamgambo hao walikamatwa wiki iliyopita baada ya utawala kuwapata wakisafirisha vilipuzi vya kutengenezewa nyumbani wakitumia gari lao.
Takriban wafungwa wengine15 walitumia fursa hiyo kutoroka jela.