Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tembo aliyekwama kwenye mafuriko kuokolewa Bangladesh
Waangalizi wa wanyamapori nchini Bangladesh wamesema wanajaribu kumuokoa Tembo aliyekwama usiku mmoja kwenye mafuriko.
Wakati wa mchana inawawia vigumu kwa sababu ya umati mkubwa wa watu wanaomtazama. Tembo jike huyo aliyefurushwa Bangladesh kutokea nchini India kwenye mafuriko ya mto wiki chache zilizopita.
Tembo huyo amesafiri zaidi ya kilomita mia moja akiwa ndani ya maji huku akiwa amedhoofu.
Mtaalamu wa wanyamapori Asim Mallik aliiambia BBC kuwa timu yake itajaribu kumtafuta tembo huyo nchi kavu wakati wa usiku ambapo hakutakuwa na umati wa watu, kabla ya hawajatulia na kumwokoa.