Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 07.08.2019: Dybala, Coutinho, Ozil, Eriksen, Llorente, Cancelo, Upamecano, Lukaku

Chanzo cha picha, Rex Features
Tottenham wamefikia makubaliano na Juventus kuhusu uhamisho wa mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 25, kwa dau la karibu £62m. (Sky Sports Italia, via Daily Mail)
Dybala anajiandaa kuanza mazungumzo ya mkataba na Tottenham kabla ya Alhamisi ambao ni muda wa mwisho uliowekwa kwa uhamisho wa wachezaji kukamilika. (Goal)
Tottenham pia wanapania kumsaini mshambuliaji wa Barcelona wa miaka 27- Mbrazil Philippe Coutinho. (ESPN)
DC United wanajiandaa kufanya mazungumzo na wawakilishi wa kiungo wa kati wa Arsenal Mesut Ozil, 30, wanapojaribu kujaza pengo lililoachwa wazi na Wayne Rooney anayeelekea Derby. (Mirror)

Chanzo cha picha, Getty Images
Manchester United wameongeza juhudi ya kufikia mkataba na na kiungo wa kati Tottenham Christian Eriksen, 27. (Telegraph)
Eriksen hayuko katika mpango wa wa muda mrefu wa Mauricio Pochettino, Tottenham - na tayari amethibitisha kuwa anataka changamoto mpya. (Mirror)
Uamuzi wa dakika za mwisho wa United kumhusu Eriksen unakuja licha ya tetesi ikiwa kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, ataendelea kuwa katika klabu hiyo hadi mwisho wa dirisha la uhamisho litakapofungwa. (Standard)

Chanzo cha picha, BBC Sport
United pia wanawatarajiwa kufanya uamuzi ambao haukutarajiwa kumnyakua mshambuliaji wa zamani wa Tottenham Fernando Llorente, ambaye kwa sasa yuko huru kuondoka klabu hiyo bila malipo. (Sky Sports Italy, via Metro)
Manchester City wanatarajiwa kuthibitisha usajili wa Joao Cancelo kutoka Juventus siku ya Jumatano baada ya beki huyo wa miaka 25 raia wa Ureno kupita vipimo vya kimatibabu. (Star)
Liverpool hawana mpango wa kumuuza kiungo wa kati wa Brazil Fabinho, licha ya tetesi zinazomhusisha mchezaji huyo wa miaka 25 na uhamisho wa Real Madrid. (Echo)

Chanzo cha picha, Getty Images
Crystal Palace wamekataa ofa ya £70m kutoka kwa Everton kumnunua mshambuliaji wa Ivory Coast forward Wilfried Zaha, 26.
Everton ilikuwa imewajumuisha wachezaji kama vile mshambuliaji wa Uturuki Cenk Tosun, 28, na kiungo wa kati wa Jamhuri ya Ireland James McCarthy, 28, katika ofa hiyo. (Mail)
Lakini Palace wanakaribia kufikia mkataba wa kumsajili McCarthy kutoka Everton kwa hadi £8.5m. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Getty Images
Everton wanakaribia kumsaini kwa mkopo beki wa Monaco Mfaransa Djibril Sidibe, 27. (Mail)
Vilabu hivyo vinafanya kila juhudi kuhakikisha Barcelona haimsajili tena mchezaji wao wa zamani. (Sport)
Lukaku kwa mara nyingine amefanya mazoezi na na wachezaji wa chini ya miaka 18 wa Anderlecht siku ya Jumanne, bila idhini ya United kuwa mjini Brussels. (Mail)

Chanzo cha picha, Reuters
Mshambuliaji wa Manchester United raia wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, hajarejea kutoka Carrington kujiunga na mazoezi ya kikosi cha kwanza licha ya tetesi zinazohusiana na hatma yake ya baadae katika katika klabu hiyo. (Mirror)
Paris St-Germain imetoa ofa ya kumuuza mchezaji nyota wa Brazil Neymar, 27, kwa vilabu vya Manchester United, Juventus na Real Madrid.

Chanzo cha picha, Getty Images
Manchester United na Manchester City wametuma wataalamu wao kufuatilia mchezo wa kiungo wa kati wa Norway Hakon Evjen ,19 wakati wa mchuano wa Bodo/Glimt. (TV2 via Manchester Evening News)
Tetesi Bora Jumanne
Juventus wanajiandaa kuwapa Manchester United wachezaji watatu ili kubadilishana na kiungo Paul Pogba. (Mirror)
Mpango huo kama utafaulu, utawahusisha wachezaji Danilo, 28, na Joao Cancelo, 25. (Goal.com)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal wanaweza kuelekeza nguvu zao zote katika kumsajili beki wa kati wa RB Leipzig Mfaransa Dayot Upamecano, 20, kama mbadala wa beki wa Juventus Daniele Rugani - lakini Leipzig wanataka pauni milioni 50 ili kumuachia beki huyo. (Mirror)
Leicester haitamsajili Nathan Ake katika dirisha hili la usajili baada ya klabu ya Bournemouth kutaka dau la pauni milioni 75 kwa beki huyo raia wa Uholanzai. (Sky Sports)
Arsenal wamejaribu kufikia makubaliano na nahodha wao Laurent Koscielny - lakini beki huyo mwenye miaka 33, ambaye aligoma kusafiri na timu kwenda Marekani, pia amegoma kufanya mazungumzo na klabu. (Mirror)














