Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ujerumani yafuzu kwa Kombe la Dunia 2018
Mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia Ujerumani wamefuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka ujao nchini Urusi baada ya kulaza Ireland Kaskazini 3-1 mjini Belfast.
Sebastian Rudy alifunga bao dakika ya pili, Sandro Wagner akaongeza la pili baadaye, naye Joshua Kimmich akafunga la tatu mechi ikikaribia kumalizika.
Josh Magennis alifungia Ireland Kaskazini bao la kufutia machozi kwa kutumia kichwa dakika za lala salama.
Ujerumani wamefuzu wakiwa viongozi wa kundi lakini Ireland Kaskazini wanasalia bado na matumaini ya kufuzu kupitia mechi za muondoano za kufuzu Novemba.
Vijana hao wa Michael O'Neill watamaliza mechi zao Kundi C nchini Norway Jumapili, wakilenga kumaliza wakiwa miongoni mwa timu nane bora zitakazomaliza nafasi ya pili kati ya makundi tisa ya kufuzu.
Huenda wakahitaji alama moja Oslo kufika mechi za kufuzu za muondoano.
Droo ya mechi hizo itafanyika tarehe 17 Oktoba.