Rooney ajiunga na Everton miaka 13 tangu aihame klabu hiyo

Wayne Rooney

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wayne Rooney scored a club record 253 goals in 559 games for Manchester United

Mshambuliaji wa Manchester United na mshikilizi wa rekodi ya mabao Wayne Rooney amejiunga na Everton, miaka 13 tangu akihame klabu hiyo.

Rooney mwenye umri wa miaka 31 alichezea Manchester United mara 559 akifunga mabao 253.

Alishinda ligi tano za Primia tangu aihame Everton kwa pauni milioni 27 mwaka 2004.

Wayne Rooney

Chanzo cha picha, BBC Football

"Ninahisi vizuri kurudi, sitangoja kukutana na wenzangu, kuingia mazoezini na kisha kuingia uwanjani kucheza." alisema Rooney.

Rooney anarejea Everton waaati Man U ina mipango ya kumsajili mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku kwa pauni milioni 75.

Wayne Rooney, aged 10, in 1995

Chanzo cha picha, Rex Features

Maelezo ya picha, Wayne Rooney akiwa na miaka 10 mwaka 1995