Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Arsenal yashinda na kupanda juu ya Manchester United
Arsenal imeimarisha matumaini yao ya kutaka kuwa katika timu nne bora katika jedwali la Uingereza kufuatia ushindi wao wa mabao 2-0 dhidi ya Southampton.
Mabao hayo yalifungwa na Alexi Sanchez na Olivier Giroud.
Baada ya kipindi cha kwanza kilichokosa mchezo mzuri Sanchez aliwashangaza wengi baada ya kuwachenga walinzi wa Southampton na kisha kucheka na wavu.
Mchezaji wa ziada Giroud ambaye aliingia mahala pake Wellbeck aliimarisha ushindi huo kwa kufunga kwa kichwa muda mfupi baada ya kuingia uwanjani.
Southampton hawakufanya mashambulizi mengi katika safu ya ulinzi ya Arsenal.
Fursa yao kuu ilikuwa katika kipindi cha kwanza wakati Manolo Gabbiadini alipopiga mkwaju uliookolewa na Petr Cech.
Ushindi huo unamaanisha kwamba Arsenal inapanda juu ya Manchester United katika nafasi ya 5 ,alama tatu nyuma ya Manchester City.