Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Guardiola: Barcelona ni ''mashine''
Barcelona ni ''mashine'' ambayo huenda ikatawala mechi dhidi ya Manchester City siku ya jumatano ,kulingana na Pep Guardiola.raia huyo wa Uhispania alishinda kombe la Ulaya akiwa mchezaji na kocha wakati alipokuwa akiiongoza timu hiyo la La Liga.
Ataelekea tena Nou Camp katika mechi ya vilabu bingwa Ulaya wiki ijayo akijua kibarua kigumu kinachoisubiri timu yake.
''Barcelona ni timu maalum kutokana na mchezo wao,Ni mashine'',alisema.
''Itachukua muda mrefu kuweza kufikia kiwango cha Barcelona,Muongo mmoja uliopita,miaka 50 iliopita Barcelona imekuwa ikitawala katika soka'' .
''Napenda wanavyocheza'',aliongezea.''Wana wachezaji watatu wazuri sana -lionel Messi,Luis Suarez na Neymar mbele.ni washambuliaji hatari.Wana timu nzuri''.