Habari za hivi punde, Wahouthi nchini Yemen: Tumeishambulia Israeli mara tatu, na zaidi yanakuja

Chanzo cha picha, Telegram/Yahya Saree
Kama tunavyoripoti kwamba kuna vurugu katika eneo lote la Ukanda wa Gaza, katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa, kwenye mpaka wa Israeli na Lebanoni, na mahali kwengine.
Sasa, Wahouthi nchini Yemen - mamia ya maili kusini-mashariki mwa Israeli - wanathibitisha kuwa tayari wamerusha "idadi kubwa" ya makombora ya balestiki na drones kuelekea Israeli.
Kama tulivyoripoti hapo awali, ving'ora vya mashambulizi ya anga vilisikika katika mji wa Eilat kusini mwa Israel siku ya Jumanne baada ya "uvamizi mkali wa ndege", ambao Israel ilidungua kwenye Bahari Nyekundu.
Msemaji wa jeshi la Houthis Yahya Saree alisema katika taarifa yake kwa njia ya televisheni kuwa ni operesheni yao ya tatu inayolenga Israel - na kwamba zaidi yatafuata.Vikosi vya Houthi "vitaendelea kufanya operesheni maalum hadi uvamizi wa Israel utakapomalizika," Saree alisema.
Wiki iliyopita, Israel ilishutumu kundi la waasi la Yemen wanaoungwa mkono na Iran kwa kutuma ndege zisizo na rubani ambazo zilisababisha milipuko katika miji miwili ya Misri - ikisema zilinuiwa kuishambulia Israel.






















