Shirika la
Umoja wa Mataifa linakabiliwa na tishio la 'kuporomoka kiuchumi' kutokana na
mataifa wanachama kukosa kulipa ada zao kwa shirika hilo.
Katibu Mkuu
wa Mmoja wa Mataifa António Guterres, amesema shirika hilo linakumbwa na uhaba
wa fedha, hali ambayo inahatarisha utoaji wa huduma, na fedha walizonazo huenda
zikaisha ifikiapo mwezi Julai.
Guterres
aliwaandikia mabalozi wa mataifa wanachama 193 akiwataka kuheshimu wajibu wao
wa kutoa malipo kwa shirika hilo, ili kuizuia kuporomoka kwake.
Tangazo hili
linakuja baada ya taifa la Marekani ambalo lililokuwa mfadhili mkubwa wa
shirika hilo kukataa kufadhili miradi ya kudumisha amani inayoendeshwa na umoja
wa mataifa na kujiondoa kwa mashirika mengine kwa madai ya "kuharibu pesa
za walipa kodi".
Wanachama wengine kadhaa pia wana madeni au wanakataa tu
kulipa.
Guterres
amesema umoja wa mataifa awali imekumbwa na uhaba wa fedha ila kwa sasa hali
imekuwa mbaya zaidi.
Ingawa
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa liliidhinisha mabadiliko ya sehemu katika mfumo
wake wa kifedha mwishoni mwa mwaka 2025, shirika hilo bado linakabiliwa na upungufu
mkubwa wa kifedha unaozidishwa na sheria inayomaanisha kuwa linarejesha pesa
ambazo halijawahi kupokea.
Katika makao
makuu yake mjini Geneva, mabango ya onyo kuhusu hali hiyo yamewekwa kila
mahali.
Katibu huyo
aliongezea kuwa ufanisi wa mfumo wa UN, unatokana na mataifa wanachama
kuheshimu wajibu wao wa kisheria chini ya mkataba wa umoja wa mataifa, na
kuongeza kuwa mwisho wa mwaka 2025, 77% ya malipo hayakuwa yametolewa na
mataifa wanachama kwa shirika hilo.
"Siwezi
kusisitiza vya kutosha kuhusu dharura ya hali tuliyonayo kwa sasa. Hatuwezi
tekeleza bajeti zetu bila fedha kutoka mataifa wanachama, na hatuwezi rudisha
fedha ambazo hatujawahi kupokea."
"Sijui
nielezee vipi dharura ya hali tuliyonayo kwa sasa. Hatuwezi kutekeleza bajeti zetu
bila fedha, wala kurudisha fedha ambazo hatujawahi kupokea kamwe".
Mwezi
Januari, Marekani ilijiondoa kutoka mashirika tofauti ikiwemo 31 ya umoja wa
mataifa.