Rais Museveni akiri wanaharakati wa Kenya walikamatwa Uganda

Kiongozi huyo wa muda mrefu wa Uganda anayalaumu "makundi ya kigeni" kwa kuchochea machafuko.

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga na Ambia Hirsi

  1. Museveni akiri wanaharakati wa Kenya walikamatwa Uganda

    Nicholas Oyoo (kushoto) na Bob Njagi (kulia) walilakiwa na wafuasi walipowasili katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, Jumamosi.

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Nicholas Oyoo (kushoto) na Bob Njagi (kulia) walilakiwa na wafuasi walipowasili katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, Jumamosi.

    Rais wa Uganda Yoweri Museveni kwa mara ya kwanza amekiri kwamba wanaharakati wawili wa Kenya waliotoweka nchini mwake kwa muda wa wiki tano walikuwa wamekamatwa.

    Mwezi uliopita, mashuhuda waliripoti kuwaona Bob Njagi na Nicholas Oyoo wakilazimishwa kuingia kwenye gari na watu ambao waliovalia sare baada ya tukio la kisiasa ambapo walikuwa wakimuunga mkono kiongozi wa upinzani nchini Uganda Bobi Wine.

    Habari za kutekwa kwao zilithibitishwa Jumamosi lakini hadi kufikia wakati huo mamlaka ilikuwa imekanusha kuwa wanazuiliwa.

    Katika mahojiano ya moja kwa moja Jumamosi jioni, Museveni aliwataja wanaharakat hao wawili kama "wataalamu wa ghasia" ambao walikuwa wamefungiwa kwenye ''jokofu kwa siku kadhaa.''

    Museveni alikuwa akijibu swali kuhusu maandamano yaliyoongozwa na vijana katika taifa jirani la Tanzania.

    Rais huyo ambaye ameongoza Uganda kwa miongo minne aliyashutumu makundi ya kigeni kwa kuchochea ghasia na kusema "wale watakaofanya mchezo huo hapa Uganda watakiona cha mtema kuni".

    Bila ya kutaja majina, aliongeza kuwa wanaharakati wawili wa Kenya waliachiwa huru baada ya kupigiwa simu na "baadhi ya viongozi wa Kenya" waliokuwa wakisinikiza kuachiwa kwao.

    Siku ya Jumamosi, shirika la Vocal Africa lilithibitisha kuwa wanaharakati hao wawili walikuwa salama, na kwamba wako safarini kutoka Busia nchini Uganda kuelekea mji mkuu wa Kenya, Nairobi.

    "Wacha wakati huu uashirie mabadiliko muhimu katika udumishaji wa haki za binadamu katika eneo la Afrika Mashariki mahali popote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki," shirika hilo liliandika kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Jeshi la Uingereza kusaidia kulinda Ubelgiji baada ya uvamizi wa ndege zisizo na rubani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wanajeshi wa Uingereza na vifaa vyao vinatumwa nchini Ubelgiji kusaidia kuimarisha ulinzi wa baada ya uvamizi wa ndege zisizo na rubani unazoshukiwa kutekelezwa na Urusi.

    Mkuu mpya wa jeshi la Uingereza, Sir Richard Knighton, ameiambia BBC Jumapili akiwa na Laura Kuenssberg kwamba mwenzake wa Ubelgiji aliomba usaidizi mapema wiki hii na vifaa hivyo na wafanyakazi wako njiani kuelekea huko.

    Uwanja mkuu wa ndege wa Zavantem nchini Ubelgiji ulilazimika kufungwa kwa muda Alhamisi usiku baada ya ndege zisizo na rubani kuonekana juu ya anga lake.

    Ndege hizo iiazilionekana katika maeneo mengineya nchi, ikiwa ni pamoja na kambi ya kijeshi.

    Sir Richard alisema haijulikani ikiwa uvamizi huo ulikuwa wa Urusi, lakini akaongeza kuwa kuna "unawezekana" zilikuwa zinatekeleza amri ya Moscow.

    Maelezo zaidi:

  3. Mamia wahamishwa Ufilipino kabla ya kimbunga Fung-wong kutua

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Zaidi ya watu 900,000 wamehamishwa nchini Ufilipino kabla ya kimbunga Fung-wong kutua Jumapili jioni.

    Kimbunga hicho kinasafiri kwa kilomita 185 kwa saa (115mph) kikiandamana na upepo unaovuma kwa kasi ya 230km/h (143mph), kulingana na mamlaka ya hali ya hewa nchini.

    Eneo la mashariki la Bicol lilikuwa sehemu ya kwanza ya Ufilipino kuathiriwa moja kwa moja na dhoruba hiyo Jumapili asubuhi, huku Luzon likitarajiwa kukumbwa na kimbunga hicho Jumapili usiku.

    Kimbunga Fung-wong - ambacho kinajulikana kama Uwan huko Ufilipino - kinatua siku chache baada ya dhoruba ya awali, Kalmaegi, vifo vya watu 200 na kusababisha uharibifu mkubwa.

    Shule kadhaa zimesitisha masomo siku ya Jumatatu au kuzihamisha mtandaoni, huku takriban safari 300 za ndege zikiahirishawa.

    Fung-wong inatarajiwa kupunguza makali yake baada ya kutua katika wilaya za Baler na Casiguran, lakini kuna uwezekano wa dhoruba hiyokugeuka kimbunga itakapoelekea Luzon.

    Zaidi ya 200mm ya mvua inatarajiwa kunyesha katika maeneo ya Luzon, na kati ya mm 100 hadi mm200 mjini Manilla.

    Mvua hiyo inatarajiwa kusababisha mafuriko makubwa na maporomoko ya ardhi.

    Pia unaweza kuoma:

  4. Kijakazi wa Marekani auawa kwa kubisha hodi nyumba isiyo sahihi

    Maria Florinda Rios Perez aliuawa kwa kupigwa risasi baada ya kubisha kimakosa nyumba isiyo sahihi kwa miadi ya kufanya usafi.

    Chanzo cha picha, CBS

    Maelezo ya picha, Maria Florinda Rios Perez aliuawa kwa kupigwa risasi baada ya kubisha kimakosa nyumba isiyo sahihi kwa miadi ya kufanya usafi.

    Maafisa nchini Marekani wanatathmini iwapo watawasilisha mashtaka dhidi ya mwenye nyumba wa Indiana ambaye alimpiga risasi na kumuua mjakazi ambaye alibisha kimakosa nyumba isiyo sahihi.

    Polisi wanasema walimpata Maria Florinda Rios Perez akiwa amekufa mbele wa nyumba hiyo siku ya Jumatano muda mfupi kabla ya 0700 saa za ndani (12:00 GMT).

    Awali polisi walikimbilia eneo la tukio baada ya wenyeji kupiga ripoti kuhusu uwezekano wa uvamizi kwenye kitongoji cha Indianapolis cha Whitestown.

    Wawili hao hawakuonekana kuingia ndani ya nyumba hiyo, polisi walisema kwenye taarifa.

    Wamewasilisha kesi hiyo rasmi kwa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Kaunti ya Boone ili ikaguliwe ili kubaini iwapo mashtaka ya uhalifu yataanziswa rasmi.

    Polisi hawajatoa majinia ya watu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo au mtu aliyefyatua risasi, wakisema katika taarifa siku ya Ijumaa kwamba ni "suala lenye utata ambalo bado linaendelea, ni hatari kutoa maelezo zaidi kuhusu tukio hilo".

    Walihimiza uvumilivu, wakionya "kuhusu kuenea kwa habari potofu mtandaoni" kuhusu kesi hiyo.

    Mauricio Velazquez, aliiambia CBS News, mshirika wa BBC wa Marekani, kwamba anatapigania haki ya mke wake mwenye umri wa miaka 32.

    Taarifa zaidi zinasema alikuwa mama wa watoto wanne na asili yake ni Guatemala.

  5. Marekani itasusia mkutano wa G20 nchini Afrika Kusini - Trump

    Rais wa Marekani Donald Trump

    Chanzo cha picha, EPA

    Donald Trump amesema Marekani haitahudhuria mkutano wa kilele wa G20 nchini Afrika Kusini kutokana na madai yaliyokanushwa kuwa Wazungu wanateswa nchini humo.

    Rais wa Marekani alisema ni "aibu kubwa" kwamba Afrika Kusini ni mwenyeji wa mkutano huo, ambapo viongozi kutoka mataifa yenye uchumi mkubwa zaidi duniani watakusanyika mjini Johannesburg baadaye mwezi huu.

    Wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini ilielezea uamuzi wa Ikulu ya White House kuwa "wa kusikitisha", wakati msemaji wa wizara ya mambo ya nje, Chrispin Phiri, aliiambia BBC kwamba mafanikio ya mkutano huo "hayatategemea nchi moja mwanachama".

    Hakuna chama chochote cha kisiasa nchini Afrika Kusini kinachodai kuwa kuna mauaji ya halaiki nchini Afrika Kusini.

    Akiongea na kipindi cha Newshour, Bw Phiri alisema kuwa Trump "anapanga mgogoro ... kwa kutumia historia chungu ya ukoloni wa Afrika Kusini". Pia alisema "hakuna ushahidi unaothibitisha kuwa Wazungua wanateswa nchini Afrika Kusini", na kuongeza: "Afrika Kusini ina matatizo yake na tunayashughulikia. Nadhani uhalifu unaathiri kila mtu, bila kujali jamii fulani."

    "Tutaendelea bila Marekani," alisema, Bw Phiri .

    Trump aliweka ujumbe kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social akisema: "Ni aibu kubwa kwamba G20 itafanyika Afrika Kusini. "Waafrikana (watu waliotokana na walowezi wa Uholanzi, na pia wahamiaji wa Ufaransa na Wajerumani) wanauawa na mashamba yao yananyakuliwa kinyume cha sheria," aliandika.

    Maelezo zaidi:

  6. Al-Sharaa kuwa rais wa kwanza wa Syria kuzuru Ikulu ya Marekani katika kipindi cha miaka 80

    Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amewasili Washington kwa ziara rasmi.

    Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amewasili Marekani (Jumamosi usiku) kwa ziara rasmi ya kihistoria, kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Syria, siku moja baada ya Washington kuliondoa jina lake kwenye orodha yake ya magaidi.

    Saa chache kabla ya kuwasili kwake katika mji mkuu wa Marekani taarifa ziliibuka kuwa vyombo vya usalama vya Syria vimewakamata makumi ya watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa kundi linalojiita Islamic State.

    Al-Sharaa anatarajiwa kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump katika Ikulu ya White House siku ya Jumatatu, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina hiyo kufanywa na rais wa Syria tangu nchi hiyo ilipopata uhuru wake mwaka 1946.

    Juhudi za pamoja za kukabiliana na mabaki ya kundi hilo nchini Syria zinatarajiwa kuwa ajenda kuu wakati wa mazungumzo ya Sharaa na Trump.

    Al-Sharaa alikutana kwa mara ya kwanza na Trump katika mji mkuu wa Saudia, Riyadh, wakati wa ziara ya kikanda ya rais huyo wa Marekani mwezi Mei.

    Mjumbe wa Marekani nchini Syria, Tom Barrack, mapema mwezi huu alisema kwamba Al-Sharaa itatia saini makubaliano ya kujiunga na muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani dhidi ya kundi la Islamic State.

    Chanzo cha kidiplomasia nchini Syria kiliiambia shirika la habari la AFP kwamba Marekani inapanga kuanzisha kituo cha kijeshi karibu na mji wa Damascus "kuratibu misaada ya kibinadamu na kufuatilia hali kati ya Syria na Israel."

    Vyanzo vinavyofahamu suala hilo vililithibitishia shirika la habari la Reuters hapo awali kwamba Washington inajiandaa kupeleka wanajeshi katika kambi ya wanahewa mjini Damascus ili kusaidia utekelezaji wa makubaliano ya kiusalama kati ya Syria na Israel ambayo yaliyosimamiwa na Marekani.

    Trump na al-Sharaa pia wamepangwa kujadili mazungumzo ya moja kwa moja kati ya mamlaka ya Syria na Israel.

    Pia unaweza kusoma:

  7. Watu sita wafariki huku Urusi ikishambulia maeneo ya nishati na makazi Ukraine

    Athari za mashambulizi

    Chanzo cha picha, Reuters

    Takribani watu sita wamefariki baada ya Urusi kushambulia kwa mamia ya makombora na ndege zisizo na rubani kwenye miundombinu ya nishati na makazi nchini Ukraine usiku kucha.

    Shambulio kwenye jengo la ghorofa katika jiji la Dnipro liliwaua watu wawili na kuwajeruhi 12, huku watatu wakifariki huko Zaporizhzhia.

    Kwa jumla, maeneo 25 kote Ukraine, ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa Kyiv, yalipigwa, na kuacha maeneo mengi bila umeme na joto.

    Waziri Mkuu Yulia Svyrydenko alisema kwenye Telegram kwamba vituo vikubwa vya nishati viliharibiwa katika maeneo ya Poltava, Kharkiv na Kyiv, na kazi inaendelea ya kurejesha umeme.

    Nchini Urusi, wizara ya ulinzi ilisema vikosi vyake vilipiga ndege zisizo na rubani 79 za Ukraine usiku kucha.

    Jeshi la anga la Ukraine lilisema Urusi ilikuwa imerusha zaidi ya ndege zisizo na rubani 450 zenye milipuko na makombora 45.

    Makombora tisa na ndege zisizo na rubani 406 ziliripotiwa kuangushwa.

    Wizara ya Nishati ya Ukraine ilisema kulikuwa na kukatika kwa umeme katika maeneo ya Dnipropetrovsk, Chernihiv, Zaporizhzhya, Odesa na Kirovohrad, lakini kazi ya ukarabati inaendelea.

    Svyrydenko alisema miundombinu muhimu tayari imeunganishwa tena, na usambazaji wa maji unadumishwa kwa kutumia jenereta.

    Unaweza kusoma;

  8. Zaidi ya safari za ndege 1,400 zafutwa huku hatua ya kupunguzwa kwa safari ikiingia siku ya pili Marekani

    Abiria

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Zaidi ya safari za ndege 1,400 kwenda, kutoka, au ndani ya Marekani zilifutwa Jumamosi baada ya mashirika ya ndege kuambiwa wiki hii kupunguza safari za anga wakati wa kufungwa kwa serikali ya nchi hiyo.

    Karibu safari za ndege 6,000 pia ziliahirishwa, kutoka zaidi ya safari za ndege 7,000 siku ya Ijumaa, kulingana na FlightAware inayofuatilia safari za ngege.

    Mamlaka ya Usafiri wa Anga, (FAA) ilitangaza mapema wiki hiyo kwamba itapunguza shughuli za safiri za anga kwa hadi 10% katika viwanja 40 vya ndege vyenye shughuli nyingi zaidi nchini humo, huku wadhibiti wa safari za anga, ambao wanafanya kazi bila malipo wakati wa kufungwa, wakiripoti uchovu.

    Warepublican na Wademokrat wanabaki kugawanyika kuhusu jinsi ya kumaliza mkwamo katika Bunge huku kufungwa kwa serikali, ambako kulianza Oktoba 1, kukiendelea.

    Pia unaweza kusoma:

  9. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu hii leo