Aliko Dangote arudi kileleni mwa mtu tajiri zaidi barani Afrika - Forbes

Chanzo cha picha, Getty Images
Aliko Dangote wa Nigeria anaongoza orodha hiyo kwa mwaka wa 14 mfululizo akiwa na thamani ya dola bilioni 23.9, kutoka dola bilioni 13.9 mwaka mmoja uliopita.
Ongezeko la utairi wake linatokana na Forbes kuongeza thamani ya kiwanda chake cha kusafisha mafuta, ambacho kilifunguliwa mwaka jana nje kidogo ya Lagos baada ya kuchelewa kwa muda mrefu.
Kulingana na jarida la forbes kiwanda hicho cha kusafishia mafuta kilitatizika kwa miaka mingi kuanza kutokana na mizozo ya udhibiti na vikwazo vingine, lakini kilianza kusafisha kiasi kidogo cha mafuta mapema 2024 na kinatarajiwa kufikia uwezo wake kamili mwezi huu. Hiyo imeruhusu Nigeria–nchi kubwa inayozalisha mafuta–kuanza kuuza bidhaa za petroli iliyosafishwa.
"Hii ni ahueni kubwa sana," Dangote, 67, aliiambia Forbes mwezi Februari. Dangote, ambaye sasa ni mmoja wa watu 100 tajiri zaidi duniani, anaamini kwamba mradi wake wa hivi karibuni ni “hatua muhimu katika kuhakikisha kwamba Afrika ina uwezo wa kusafisha mafuta yake ghafi, na hivyo kutengeneza utajiri na ufanisi kwa wakazi wake wengi.”
Mwafrika wa pili tajiri zaidi ni tajiri wa bidhaa za anasa wa Afrika Kusini Johann Rupert, ambaye utajiri wake ulipanda kwa 39% hadi $ 14 bilioni, faida ya pili kwa ukubwa kati ya mabilionea.
Rupert ameshikilia nafasi ya 2 tangu 2022.
Ifuatayo ni orodha ya watu 10 matajiri Afrika.
10. Patrice Motsepe











