FIFA imejiharibia yenyewe kwa mpango wa Kombe la Dunia - Mkuu wa Ligi Kuu ya Uingereza

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Mtendaji mkuu wa Ligi Kuu ya England, Richard Masters amekosoa mpango wa Rais wa shirikikisho la soka duniani Fifa, Gianni Infantino wa kuuza hisa za Kombe la Dunia, akisema shirikisho hilo "limebonyeza kitufe cha kujiangamiza.
Infantino yuko chini ya shinikizo kubwa kuhusu jaribio lake, ambalo baadaye lilishindikana, la kuunda kampuni mpya ya kusimamia haki za kibiashara na tiketi za mashindano yote ya Fifa, ikiwa ni pamoja na Kombe la Dunia, huku asilimia 21 ikipangwa kuuzwa kwa kampuni bnafsi ya uwekezaji.
Mpango wa Fifa Forward Enterprise (FFE) ulisitishwa baada ya ukosoaji mkubwa wa mashirikisho kadhaa, yanayoongozwa na Uefa, ambayo yametishia kususia mashindano yote ya Fifa.
Masters aliunga mkono uamuzi wa Shirikisho la Soka la England (FA) kuondoa uungwaji mkono wake kwa Infantino, na akatoa wito wa kupatikana kwa mgombea mpya wa urais wa FIFA ambaye anaweza kuiunganisha dunia ya soka.
Soma Zaidi Hapa:



























