Trump apiga kura huko Florida huku mamilioni wakimpigia kura rais ajaye wa Marekani

Baada ya kampeni kali ya miezi kadhaa kati ya Kamala Harris na Donald Trump, Marekani itachagua rais wake ajaye.

Muhtasari

  • Wauaji wa mwanariadha wa Uganda wahukumiwa kifungo cha miaka 35
  • Uchaguzi wa Marekani 2024: Tunachojua kufikia sasa
  • Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amfuta kazi waziri wa ulinzi Gallant
  • Waziri wa Georgia asema vitisho vya mabomu vilitoka Urusi
  • FBI yatoa onyo jingine kuhusu video ghushi za uchaguzi
  • 'Acha kuzungumzia hilo': Trump akwepa swali la kura ya utoaji mimba
  • Harris awataka Wamarekani 'kutoka na kupiga kura' katika mahojiano ya redio
  • Trump apiga kura katika eneo la Palm Springs akiwa na mkewe Melania
  • Vitisho vya uwongo vya mabomu vyasababisha wapiga kura kuhama Georgia
  • Bangladesh yaimarisha malipo kwa kampuni ya Adani kuzuia kukatwa kwa usambazaji umeme
  • Mgomo wa wanyakazi wa Boeing wamalizika
  • Kesi ya kukatwa kichwa kwa mwalimu aliyeonyesha katuni ya Mtume Muhammad yaanza kusikilizwa
  • Equtoarial Guinea kuwachukulia hatua wafanyakazi wa umma waliofanya mapenzi ofisini
  • Elon Musk anaweza kuendelea kutoa $1m kwa wapiga kura, jaji aamua
  • Urusi ni 'tishio kubwa zaidi' kwa uchaguzi wa Marekani
  • Iran yahimizwa kumwachilia mwanamke aliyevua nguo chuo kikuu
  • Trump na Harris wafanya mikutano yao katika majimbo muhimu
  • Idadi ya waliopiga kura mapema Marekani yapita milioni 81

Moja kwa moja

Na Asha Juma,Lizzy Masinga & Dinah Gahamanyi

  1. Wauaji wa mwanariadha wa Uganda wahukumiwa kifungo cha miaka 35

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Benjamin Kiplagat alishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya Rio 2016, na vile vile London na Beijing kabla ya hapo.

    Kenya imewahukumu wanaume wawili kifungo cha miaka 35 kila mmoja kwa mauaji ya mwanariadha wa Uganda Benjamin Kiplagat mwishoni mwa mwaka jana.

    Mkimbiaji huyo wa mbio za kuruka viunzi kwenye Olimpiki aliuawa kwa kuchomwa kisu mkesha wa Mwaka Mpya katika mji wa Eldoret, unaojulikana kama kituo kikuu cha mafunzo kwa wanariadha.

    "Matendo yako yalikuwa ya kikatili kwa mtu asiyeweza kujitetea ambaye ulikatisha maisha yake," Jaji Reuben Nyakundi aliambia Peter Ushuru Khalumi na David Ekai Lokere wakati wa kusikizwa kwa hukumu katika Mahakama Kuu ya Eldoret.

    Mauaji ya Kiplagat yalishtua watu nchini Kenya, ambayo imeshuhudia mauaji ya wanariadha wengine kadhaa katika miaka ya hivi karibuni.

    Tangazo

    Hakimu alisema kuwa Khalumi na Lokere walimfuata Kiplagat aliyekuwa ndani ya gari lake, na kisha picha za CCTV zilionyesha kuwa walimuua kimakusudi katika hatua iliyopangwa. Sababu haswa ya mauaji hayo haikujulikana lakini wakati wa kukamatwa polisi walikuwa wamesema ni wizi.

    Mnamo Jumatatu, katika ombi la hisia kwa mahakama, mamake mwanariadha huyo alimtaka Hakimu Nyakundi atoe kifungo cha maisha.

  2. Habari za hivi punde, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amfuta kazi waziri wake wa ulinzi Yoav Gallant

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na waziri wa Ulinzi Yoav Gallant

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amemfuta kazi waziri wa ulinzi Yoav Gallant akisema kuna "mgogoro wa kuaminiana" kati yao.

    Netanyahu alisema katika taarifa kwamba imani yake kwa Gallant "imepungua" katika miezi ya hivi karibuni.

    Waziri wa Mambo ya Nje Israel Katz atachukua nafasi ya Gallant, Netanyahu aliongeza.

    Gallant alichapisha kwenye mitandao ya kijamii kwamba "usalama wa taifa la Israel ulikuwa na utabaki kuwa dhamira ya maisha yangu daima".

    Katika taarifa yake, Netanyahu alisema: "Katikati ya vita, zaidi ya hapo awali, uaminifu kamili unahitajika kati ya waziri mkuu na waziri wa ulinzi.

    "Kwa bahati mbaya, ingawa katika miezi ya kwanza ya kampeni kulikuwa na uaminifu kama huo na kulikuwa na kazi yenye matunda, katika miezi ya hivi karibuni uaminifu huu ulivunjika kati yangu na waziri wa ulinzi."

    Netanyahu alisema kuwa "mapengo makubwa yaligunduliwa kati yangu na Gallant katika usimamizi wa kampeni".

    “Mapengo haya yaliambatana na kauli na vitendo vinavyokinzana na maamuzi ya serikali na maamuzi ya baraza la mawaziri,” aliongeza.

    Netanyahu alisema "alifanya majaribio mengi ya kuziba mapengo haya, lakini yaliendelea kuwa mapana".

    Gallant alichapisha ujumbe mfupi tu kwenye X, akisema kwamba usalama wa Israeli "ulikuwa na utabaki kuwa dhamira ya maisha yangu kila wakati".

    Katz atamrithi Gallant kama waziri wa ulinzi, huku Gideon Sa'ar akiwa waziri mpya wa mambo ya nje, Netanyahu alisema.

  3. Habari za hivi punde, Uchaguzi wa Marekani 2024: Tunachojua kufikia sasa

    Waandishi wetu wamekuwa wakisafiri tangu usiku wa manane nchini Marekani kuwapasha kuhusu matokeo ya uchaguzi, na haya ndiyo yaliyotokea hadi sasa:

    • Upigaji kura sasa umeanza katika majimbo yote ya Marekani – Jimbo la Hawaii lilikuwa la hivi punde zaidi kuongezwa kwenye orodha hiyo.
    • Muda mfupi uliopita, Donald Trump alipiga kura huko Palm Beach, Florida, akiwa na mkewe Melania. Alizungumza na waandishi wa habari na kusema "tunaendelea vizuri sana"
    • Kamala Harris tayari amepiga kura - alituma kura yake kwa njia ya posta wiki iliyopita
    • Kumekuwa na masuala ya kiufundi yaliyoripotiwa katika Kaunti ya Cambria, Pennsylvania, kwani masuala ya programu yaliathiri vikaguzi vya upigaji kura. Saa za kupiga kura zimeongezwa kwa sababu ya ucheleweshaji uliosababishwa
    • Huko Georgia, kulikuwa na vitisho vitano vya mabomu visivyo vya kuaminika katika maeneo ya kupigia kura katika jimbo lote, na kusababisha uhamishaji wa wapiga kura katika maeneo mawili.
    • Maeneo mawili ya kupigia kura katika Kaunti ya Cobb yatasalia wazi kwa sababu ya ucheleweshaji
    • Waziri wa mambo ya nje wa Georgia aliambia wanahabari kwamba vitisho hivyo vilitoka Urusi
    • Kama ilivyo desturi, kura za kwanza zilipigwa na wakazi sita wa Dixville Notch, New Hampshire, usiku wa manane saa za huko, na watatu walimpigia kura Trump huku watu watatu waliosalia wakipimpigia kura Harris .
    • Na kura za maoni zinaonyesha kuwa Harris amechukua uongozi katika jimbo kuu la Pennsylvania, na ana uongozi mdogo huko Wisconsin na Michigan.
    • Wakati huo huo Trump bado ana uongozi mdogo huko Nevada, Georgia, North Carolina, na Arizona
  4. Waziri wa Georgia asema vitisho vya mabomu vilitoka Urusi

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Georgia Brad Raffensperger

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Georgia Brad Raffensperger anasema vitisho vya bomu vilivyotolewa dhidi ya maeneo mengi ya kupigia kura asubuhi ya leo havikuwa vya kuaminika.

    Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Raffensperger anasema vitisho hivyo vilikuwa na asili ya Urusi. "Tunawapata kila wakati," anaongeza - na anasema "nia yao yote" ni kujaribu na "kuyumbisha Marekani".

    Hapo awali, tuliripoti kwamba vitisho vitano tofauti vilitolewa katika maeneo ya kupigia kura katika Kaunti ya Fulton.

    Vituo viwili vilihamishwa, lakini vyote vimefunguliwa tena na upigaji kura unaendelea.

  5. Habari za hivi punde, FBI yatoa onyo jingine kuhusu video ghushi za uchaguzi

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Maafisa wa FBI

    FBI imetoa onyo jingine, kuhusu video ghushi zinazosambaa mtandaoni ambazo zinalenga kutilia shaka uchaguzi wa Marekani.

    Siku ya Jumanne, FBI ilisema video mbili za uwongo ziliwahimiza Wamarekani "kupiga kura kwa mbali" kutokana na tishio kubwa la ugaidi katika vituo vya kupigia kura na madai ya udanganyifu wa wapiga kura katika magereza katika majimbo kadhaa yanayogombaniwa.

    Video hizo zilihaririwa ili kuonekana kama taarifa kwa vyombo vya habari kutoka FBI na ripoti ya CBS News. Hazikupokea idadi kubwa ya maoni kwenye mtandao wa X.

    FBI ilisema video hizo zililenga "kudhoofisha mchakato wetu wa kidemokrasia na kuondoa imani katika mfumo wa uchaguzi".

    CBS News ilichapisha kwenye X, kwamba video inayotumia nembo yake "imetengenezwa".

    BBC Verify ilipata maudhui ya video hizo zinazolingana na mtandao mpana wa habari za upotoshaji wenye makao yake nchini Urusi ambao umezalisha mamia ya habari bandia katika miezi ya hivi karibuni.

  6. Habari za hivi punde, 'Acha kuzungumzia hilo': Trump akwepa swali la kura ya utoaji mimba

    Florida ni miongoni mwa majimbo 10 ya Marekani yenye kipimo cha kura kuhusu utoaji mimba.

    Wapiga kura wanafikiria iwapo watabatilisha marufuku ya kuavya mimba ya wiki sita inayotekelezwa kwa sasa na kufikia kiwango cha uwezo wa kijusi, ambao ni takriban wiki 24 za ujauzito.

    Donald Trump ameulizwa jinsi alivyopiga kura kuhusu suala hilo baada ya kupiga kura yake huko Florida muda mfupi uliopita. "Acha tu kuzungumza juu ya hilo", alijibu.

    Ni kielelezo wazi cha jinsi ambavyo mara nyingi amekuwa akihangaika kushughulikia suala la utoaji mimba. Mnamo Agosti, Trump alikabiliwa na upinzani kutoka kwa wahafidhina baada ya kuonekana kuunga mkono hatua ya kura - na siku iliyofuata, alisema angepiga kura dhidi yake.

    Mpinzani wake, Kamala Harris, pia amekwepa kuhusu hatua ya kura katika jimbo lake la California, ambayo itaongeza hukumu kwa uhalifu fulani wa dawa za kulevya na wizi.

    "Sitazungumza juu ya kura hiyo kwa sababu, kusema kweli, ni Jumapili kabla ya uchaguzi na sitaki kutoa idhini kwa njia moja au nyingine," alisema.

  7. Harris awataka Wamarekani 'kutoka na kupiga kura' katika mahojiano ya redio

    Harris awataka Wamarekani 'kutoka na kupiga kura' katika mahojiano ya redio

    Mgomnbea wa urais kjupitia tiketi ya Demcrats Kamala Harris amewahimiza Wamarekani "kujitokeza na kupiga kura" katika mahojiano machache ya redio leo.

    "Lazima tuifanye. Leo ni siku ya kupiga kura, na watu wanahitaji kutoka na kupiga kura," anasema kwenye kituo cha Atlanta WVEE-FM.

    Alipoulizwa kuhusu jinsi urais wake unavyoweza kuweka historia kwenye The Big Tigger Morning Show huko Georgia, Harris anasema amekuwa akizingatia "kazi iliyo mbele yangu" na kuhakikisha kuwa "anajibu mahitaji ya watu karibu na sera, "kulingana na mshirika wa BBC wa Marekani CBS News.

  8. Habari za hivi punde, Trump apiga kura katika eneo la Palm Springs akiwa na mkewe Melania

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Trump na mkewe Melania

    Hivi sasa rais wa zamani Donald Trump anazungumza na waandishi wa habari huko Palm Springs, Florida, anapopiga kura katika uchaguzi huo. Ameungana na mke wake, Melania.

    Akiwa amevalia kofia yake nyekundu, anazungumza na vyombo vya habari sasa.

    "Ninajiamini sana...na inaonekana Republicans wamejitokeza kwa nguvu," anasema.

    Trump anasema "aliheshimiwa" kuona kwamba mistari ya wapiga kura ni mirefu sana.

    "Tulirudi usiku wa kuamkia jana," anasema, akizungumzia mkutano wake wa Michigan

  9. Vitisho vya uwongo vya mabomu vyasababisha wapiga kura kuhama Georgia

    .

    Chanzo cha picha, EPA-EFE/REX/Shutterstock

    Maelezo ya picha, Mpiga kura anajitayarisha kukagua kura yake huko Atlanta, Kaunti ya Fulton

    Kulikuwa na vitisho vitano vya mabomu visivyoaminika katika maeneo ya kupigia kura katika Kaunti ya Fulton, Georgia, asubuhi ya leo, kulingana na CBS, mshirika wa BBC wa Marekani.

    Nadine Williams, mkurugenzi wa usajili na uchaguzi wa kaunti hiyo, anasema vitisho hivyo vilisababisha kuhamishwa kwa muda kwa maeneo mawili kwa takriban dakika 30 kila moja katika jimbo linaloshindaniwa.

    Kaunti hiyo, inayojumuisha jiji la Atlanta, sasa inatafuta amri ya mahakama ya kuongeza muda wa maeneo mawili yaliyoathiriwa hadi 19:30 saa za ndani (00:30 GMT Jumatano).

    Tuliripoti mapema kwamba masuala ya kiufundi katika Kaunti ya Cambria, Pennsylvania, yalikuwa yamewazuia baadhi ya wapigakura kuchanganua kura zao, na afisa wa uchaguzi katika jimbo hilo linalogombaniwa pia aliwasilisha amri ya mahakama ya kuongeza muda wa kupiga kura.

  10. Kambi ya Trump yadai maafisa wa uchaguzi 'walifukuzwa kinyume cha sheria'

    Kituo cha kura

    Kambi ya mgombea wa Republican Donald Trump imedai kuwa maafisa wake wanne wa uchaguzi walizuiliwa na kufukuzwa kinyume cha sheria" katika eneo la kupigia kura huko Philadelphia leo asubuhi siku ya uchaguzi.

    "Huu ni uhalifu, na haupaswi kutokea katika uchaguzi wa haki na salama kama ilivyoahidiwa," taarifa ya kambi hiyo inaeleza "Huu ni ukiukaji mkubwa wa Imani usiokubalika, unaodhoofisha uwazi na uchaguzi wa Philadelphia.

    " Watatu kati ya wanne waliongezwa kabla, ilieleza taarifa hiyo. "Tunamtaka Mwanasheria wa eneo hili Larry Krasner na maafisa wa uchaguzi kuchukua hatua mara moja na kuruhusu waangalizi wetu wa uchaguzi" taarifa hiyo inaongeza.

    "Kutowaruhusu Warepublican kuingia katika chumba hicho kunatishia uadilifu na usalama wa uchaguzi wa Pennsylvania." Krasner, wakili wa wilaya ya Philadelphia, atafanya mkutano na waandishi wa habari ili kutoa taarifa za uchaguzi saa 10:30 kwa saa za Pennsylvania (15:30 GMT).

    Unaweza pia kusoma;

  11. Ni masuala gani mengine ambayo Wamarekani wanapigia kura leo?

    North Carolina

    Chanzo cha picha, Reuters

    Si tu chaguo kati ya Kamala Harris na Donald Trump leo, wapiga kura nchini Marekani wana mengi zaidi ya kuamua hasa:

    • Haki za uavyaji mimba: Zikokwenye kura katika majimbo 10, ikiwa ni pamoja na majimbo ya Arizona na Nevada.
    • Theluthi moja ya Seneti ya Marekani- viti 34 kati ya viti 100 pia vinawaniwa.
    • Wanademokrasia kwa sasa wanadhibiti Seneti kwa tofauti ya kiti kimoja
    • Katika Baraza la Wawakilishi la Marekani, baraza la chini la Congress, viti vyote 435 vinatarajiwa kuchaguliwa, kama inavyofanyika kila baada ya miaka miwili.
    • Utumiaji wa bangi kama kiburudisho au matibabu: Pia uko kwenye kura katika majimbo manne - Florida, Nebraska, North Dakota na South Dakota.
    • Kura za maoni kuhusu upigaji kura na uchaguzi: Katika baadhi ya maeneo, wapiga kura pia watachagua jinsi wanavyotaka uchaguzi wao uendeshwe.
  12. Uchaguzi Marekani 2024: Mwongozo kuhusu wagombea

    Trump. Kamala

    Kamala Harris: Makamu wa Rais

    Umri: miaka 60

    Chama: Democratic Party

    Ahadi za kampeni: Maneno ya Harris ni "Haturudi nyuma", akimaanisha sera za rais wa zamani Donald Trump.

    Anaunga mkono haki za uavyaji mimba, amezindua mpango wa kiuchumi wa kupiga marufuku upandishaji wa bei za bidhaa, na anasema "atakomesha uhaba wa nyumba wa Marekani".

    Wakati muhimu wa 2024: Hotuba yake kuu katika Kongamano la Kitaifa la Kidemokrasia mnamo Agosti, takribani mwezi mmoja baada ya Joe Biden kujiondoa kwenye kinyang'anyiro.

    Donald Trump,Rais wa zamani wa Marekani

    Umri: 78

    Chama: Chama cha Republican

    Ahadi za kampeni: Trump anasema "atafunga mpaka" kuwakomesha wahamiaji haramu, ameahidi kupunguzwa kwa ushuru, kupendekeza ushuru wa 10% kwa bidhaa zote za Marekani na kuapa kupunguza gharama za nishati.

    Wakati muhimu wa 2024: Kunusurika na jaribio la mauaji huko Butler, Pennsylvania, picha ya kudumu ambayo ilimuonesha akiwa na damu usoni.

    Unaweza kusoma;

  13. Uchaguzi wa Marekani 2024: Mshindi atatangazwa lini? Na maswali mengine muhimu yajibiwa

    Siku ya uchaguzi nchini Marekani imefika, kwa hivyo sasa ni wakati mzuri kama wa kujikumbusha jinsi kinyang’anyiro hiki kinavyofanyika.

    Je, unashindaje?

    Rais ajaye wa Marekani huamuliwa na mgombea gani atashinda kura nyingi katika wawakilishi maalumu wanaopiga wa majimbo wanaopiga kura ya urais . Kila jimbo limetengewa idadi ya kura za cwawakili wa uchaguzi kulingana na idadi ya watu wake. kote Marekani kuna kura 538 za wawakilishi wa maalumu wa uchaguzi kwa jumla. Katika majimbo 48 kati ya 50, mgombea atakayeshinda kura nyingi zaidi za mtu binafsi hutunukiwa kura zake zote za wawakilishi maalumu wa majimbo wanaopiga kura ya urais. Mgombea aliyeshinda anahitaji kupata idadi kubwa ya hizo - kwa hivyo angalau 270.

    Tutajua lini mshindi?

    Hili ni swali gumu, na jibu - "linategemea" . Baadhi ya majimbo yanaweza kubadilisha matokeo haraka sana, lakini kwa unaweza kuwa mchakato mrefu - haswa ikiwa kuna idadi kubwa ya kura za mapema na za barua-pepe ambazo huhesabiwa usiku baada ya zile zilizopigwa ana kwa ana. Katika uchaguzi uliopita wa rais wa Marekani mwaka 2020, hakutangazwa hadi Jumamosi baada ya siku ya kupiga kura ambapo vyombo vya habari vya Marekani vilikuwa na uhakika wa kutosha kutangaza matokeo.

    Mshindi atachukua linii mamlaka?

    Jambo moja tunalojua ni kwamba yeyote atakayeshinda hawi rais hadi siku ya kuapishwa - atakapoapishwa nje ya Ikulu ya Marekani huko Washington DC na jaji mkuu wa Mahakama ya Juu. Siku hiyo ni Jumatatu tarehe 20 Januari 2025.

  14. Afariki dunia baada ya kupanda mlima Himalaya

    Mpanda mlima

    Chanzo cha picha, Ondrej Huserka / Facebook

    Mpanda mlima maarufu wa Slovakia amepoteza maisha alipokuwa akishuka kilele cha mita 7,234 (23,730ft) huko Nepal, baada ya kukamilisha kazi adimu ya kupanda mlima huo hatari wa mashariki.

    Ondrej Huserka alianguka kwenye siku ya Alhamisi, baada ya yeye na mshirika wake, Lantang Lirung kupanda mlima Himalaya, kilele cha 99 juu zaidi duniani.

    Mpanda milima huyo mwenye umri wa miaka 34 hapo awali alikuwa amepanda milima ya Alps, Patagonia na Pamir.

    Mshirika wake wa Kicheki Marek Holecek alisema kuwa wawili hao walikuwa wakirejea kambini baada ya kuwa wapanda milima wa kwanza kupanda Lantang Lirung kupitia njia "ya kutisha" ya mashariki.

    Wakati akirudisha ukuta wa mlima, kamba ya Bw.Huserka ilikatika na akaanguka kwenye shimo la barafu, alisema mshirika wake. Kisha "aligonga uso wenye pembe baada ya kushuka kwa 8m, kisha akaendelea chini ndani ya kina cha barafu".

    Katika chapisho la Facebook lenye hisia kali, Bw Holecek alikumbuka kusikia kilio cha mwenzake akiomba msaada na akijaribu sana kumwokoa.

    Baada ya kumkomboa kutoka kwenye barafu, Bw Holecek aligundua kuwa alikuwa amepooza. "Nyota yake ilikuwa inafifia alipokuwa amelala mikononi mwangu," alisema.

    Chama cha wapanda mlima wa Slovakia, SHS James, kilisema hali mbaya ya hewa nchini Nepal imetatiza shughuli za uokoaji.

  15. Takribani wanajeshi 10,000 wa Korea Kaskazini wako katika eneo la Kursk nchini Urusi - Pentagon

    Wanajeshi

    Chanzo cha picha, ED JONES/AFP

    Kati ya wanajeshi 11,000 na 12,000 kutoka Korea Kaskazini tayari wamewasili nchini Urusi, ambapo takribani 10,000 wako katika eneo la Kursk, msemaji wa Pentagon Meja Jenerali Pat Ryder alisema katika kikao fupi siku ya Jumatatu.

    Hotuba yake ilitangazwa kwenye kituo cha YouTube cha wizara hiyo, Forbes inaripoti.

    Siku moja kabla, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, akinukuu data za kijasusi, alitangaza kwamba kulikuwa na wanajeshi 11,000 wa Korea Kaskazini ambao, kulingana na yeye, walikuwa katika mkoa wa Kursk, ambapo Vikosi vya Wanajeshi vya Ukrainevinaendesha operesheni za kijeshi dhidi ya jeshi la Urusi.

    Moscow haikani madai ya kuwepo kwa wanajeshi wa Korea Kaskazini nchini Urusi, lakini haisemi jinsi inavyopanga kuwatumia.

    Nchi za Magharibi zinachukulia matumizi ya wanajeshi wa Korea Kaskazini kama kuzidisha mzozo kati ya Urusi na Ukraine.

    Unaweza kusoma;

  16. Bangladesh yaimarisha malipo kwa kampuni ya Adani kuzuia kukatwa kwa usambazaji umeme

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Bangladesh inakusanya malipo ya kampuni ya umeme ya Adani baada ya kampuni hiyo ya India kukata usambazaji wa umeme kwa nusu, ikiripotiwa kuwa ni kutokana na malipo ambayo hahayajalipwa ya $800m.

    Maafisa wawili wakuu wa serikali waliiambia BBC kuwa tayari wanashughulikia baadhi ya malipo ya kampuni ya Adani, ambayo hutoa 10% ya umeme unaotumiwa na Bangladesh.

    "Tumeshughulikia matatizo ya malipo na tayari tumetoa mkopo wa $170 milioni [£143m] kwa kampuni ya Adani," afisa mkuu wa Bodi ya Umeme ya Bangladesh aliambia BBC.

    Kampuni ya Adani huipatia Bangladesh nguvu za umeme kutoka kwa kiwanda chake cha megawati 1600 kinachotumia makaa ya mawe mashariki mwa India.

    Hata hivyo, kampuni hiyo haijajibu maswali ya BBC kuhusu kupunguzwa kwa usambazaji wa umeme kwa Bangladesh, ambayo inakabiliwa na uhaba wa umeme mara kwa mara.

    Maafisa wanasema kampuni hiyo imetishia kusitisha usambazaji kabisa ikiwa pesa inayodai haitaikuwa imelipwa kikamilifu kufikia tarehe 7 Novemba.

    Lakini afisa wa Bodi ya Umeme ya Bangladesh alisema "hawafikirii kuwa itafikia hatua ambapo usambazaji wote utakatizwa".

    Maafisa wa Bangladesh waliiambia BBC watafanya malipo polepole na mara kwa mara na wana uhakika wa kusuluhisha tatizo la malipo.

  17. Mgomo wa wafanyakazi wa Boeing wamalizika

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wafanyikazi wa Boeing wamepiga kura kukubali ofa ya malipo ya hivi karibuni ya kampuni kubwa ya usafiri wa anga na kumaliza mgomo wa wiki saba.

    Chini ya mkataba mpya, watapata nyongeza ya asilimia 38% ya mishahara katika kipindi cha miaka minne ijayo.

    Wafanyakazi waliogoma wanaweza kuanza kurejea kazini kuanzia Jumatano, au hadi tarehe 12 Novemba, chama cha Kimataifa cha Wafanyabiashara na Wafanyakazi wa Anga kimesema.

    Mgomo wa takriban wafanyikazi 30,000 wa Boeing ulianza tarehe 13 Septemba, na kusababisha kupungua kwa kasi kwa mapato.

    Chama cha wafanyakazi wa Anga kilisema 59% ya wafanyikazi waliogoma walipiga kura kuunga mkono mpango huo mpya, ambao pia unajumuisha marupurupu ya mara moja ya $12,000 (£9,300), pamoja na mabadiliko ya mipango ya kustaafu ya wafanyikazi.

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

  18. Kesi ya kukatwa kichwa kwa mwalimu aliyeonyesha katuni ya Mtume Muhammad yaanza kusikilizwa

    .

    Chanzo cha picha, x.com/ch_capuano

    Watu wanane wamefikishwa mahakamani mjini Paris wakituhumiwa kuchochea mauaji ya Samuel Paty, mwalimu aliyekatwa kichwa barabarani nje ya shule yake miaka minne iliyopita kwa madai kwamba alionyesha katuni ya Mtume Muhammad.

    Abdoullakh Anzorov, kijana mwenye asili ya Chechnya ambaye alikuwa amebeba kisu, alifariki dunia. Alipigwa risasi na polisi dakika chache baada ya kufanya shambulizi.

    Kwa hivyo, kesi hiyo itaangazia zaidi hali ambayo ilisababisha mauaji, mauaji badala ya mauaji yenyewe.

    Kwa zaidi ya wiki saba, mahakama itasikiliza jinsi uwongo wa msichana wa shule mwenye umri wa miaka 13 alivyosababisha kampeni ya kimataifa ya chuki kwenye mitandao ya kijamii, na kuhamasisha dhamira ya kulipiza kisasi kutoka kwa anayejiita mtetezi wa Uislamu.

    Katika kesi hiyo ni wanaume wawili wanaoshtakiwa kwa kumtambua Bw Paty kama "kafiri" kwenye mtandao, marafiki wawili wa Anzorov ambaye inadaiwa walimpa usaidizi wa usafiri, na wengine wanne ambao walitoa usaidizi kwenye mitandao ya mawasiliano.

    Mauaji ya Bw Paty yalikuwa ya kutisha nchini Ufaransa.

    Soma zaidi:

  19. Baltasar Ebang Engonga: Equtoarial Guinea kuwachukulia hatua wafanyakazi wa umma waliofanya mapenzi ofisini

    TH

    Chanzo cha picha, Baltasar Engonga

    Mamia ya kanda za ngono zinazomhusisha mtumishi wa serikali wa ngazi ya juu wa Equatorial Guinea pamoja na wake za watu zimeenea kwenye mitandao ya kijamii, na kusababisha mamlaka kujaribu kuzuia kuenea kwa video hizo.

    Katika video hizo mkurugenzi wa Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Fedha (ANIF), Baltasar Ebang Engonga, anaonekana akiwa na wanawake mbalimbali - wakiwemo wake za maafisa mashuhuri -ofisini kwake katika wizara ya fedha.

    Siku ya Jumatatu, makamu wa rais wa nchi hiyo Teodoro Nguema Obiang Mangue alitangaza kwenye X kwamba serikali itaamuru "kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi wote wa umma ambao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi katika ofisi za wizara, kwani hii ni ukiukaji wa wazi wa kanuni za maadili na sheria ya maadili ya umma".

    Si mara ya kwanza kwa kanda za ngono zinazohusisha watumishi wa umma kuvuja kwenye mitandao ya kijamii.

    Lakini suala hilo limevuma kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea kutokana na sifa mbaya za viongozi waliohusika.

    Wiki iliyopita, Obiang alisema kuwa ametoa notisi ya saa 24 kwa wizara ya mawasiliano ya Guinea ya Ikweta, mdhibiti na makampuni ya simu "kuzuia usambazaji wa video za ngono ambazo zimejaa mitandao ya kijamii nchini Equatorial Guinea".

    "Kama serikali, hatuwezi kuendelea kuona familia zikiharibiwa," makamu wa rais anayehusika na ulinzi na usalama alisema.

    Kulingana na akaunti zilizosambazwa kwa mara ya kwanza na vikundi vya Whatsapp na kisha kuwekwa kwenye Facebook, Instagram, TikTok na X, Engonga alipiga zaidi ya video 400 za ngono ofisini kwake.

    Kanda hizo za ngono zilivujishwa kwenye mitandao ya kijamii wakati ambapo alikuwa amewekwa rumande katika gereza maarufu la Black Beach la Malabo katika kesi ya ubadhirifu wa fedha za umma, kulingana na kituo cha televisheni cha serikali TVGE.

    Mwendesha mashtaka mkuu wa Equatorial Guinea Anatolio Nzang Nguema, aliihakikishia TVGE kwamba ikiwa uchunguzi wa kimatibabu utabaini kuwa Ebang Engonga "alikuwa na ugonjwa wa zinaa" atafunguliwa mashtaka kwa kosa dhidi ya "afya ya umma".

  20. Elon Musk anaweza kuendelea kutoa $1m kwa wapiga kura, jaji aamua

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kundi la kisiasa la Elon Musk linaweza kuendelea kutoa $1m (£722,000) kwa wapiga kura katika majimbo muhimu yatakayoamua mshindi wa uchaguzi wa urais marekani , jaji ameamua.

    Zawadi ya kundi laBw Musk' la America PAC inatazamiwa kumalizika Jumanne, na mpokeaji wa mwisho tayari amebainishwa, wakili wa bilionea huyo alisema katika kikao cha mahakama siku ya Jumatatu.

    Katika hali ya kushangaza, wakili huyo alifichua kuwa watu wanaopokea pesa hizo hawakuchaguliwa kwa njia ya kubahatisha katika shindano la mtindo wa bahati nasibu, kama wengi walivyoamini, lakini walichaguliwa na kikundi.

    Wakili wa Wilaya ya Philadelphia Lawrence Krasner alikuwa ameshtaki kukomesha kile alichokiita "bahati nasibu isiyo halali" baada ya Musk kutangaza kuwa angempa mpiga kura mmoja pesa hizo kila siku hadi Siku ya Uchaguzi.

    Jaji wa Pennsylvania Angelo Foglietta hakutoa mara moja sababu ya uamuzi huo, uliotolewa saa chache baada ya kusikilizwa kwa kesi hiyo, kulingana na Associated Press.

    "Wapokeaji wa $ 1 milioni hawakuchaguliwa kwa bahati," wakili, Chris Gober, alisema wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo, kulingana na Associated Press. "Tunajua ni nani hasa atatangazwa kuwa mpokeaji wa $ 1 milioni leo na kesho."

    Bw Gober aliambia mahakama kwamba PAC tayari imeamua mpokeaji wa mwisho atakuwa mpiga kura kutoka Michigan, vyombo vya habari vya Marekani viliripoti.

    Siku ya Jumatatu, PAC ilitangaza mtu anayeitwa Joshua huko Arizona alikuwa amepewa zawai ya siku hiyo

    Soma zaidi: