Watu 10 wafariki kwa mafuriko Nairobi
Watu 10 wamethibitishwa kufariki jijini Nairobi kufuatia mafuriko makubwa yaliyokumba jiji hilo siku ya Ijumaa.
Kamanda wa Polisi jijini Nairobi George Seda alisema watu nane walisombwa na maji ya mafuriko yanayoongezeka kwa kasi, huku wengine wakifariki wakiwa ndani ya magari yaliyobebwa na mkondo wa maji.
Seda aliongeza kuwa waathiriwa wengine wawili walifariki katika matukio tofauti ya umeme wakati wa mafuriko katika sehemu tofauti za kaunti.
Aidha ameongeza kuwa, takriban magari 71 yalikwama jijini Nairobi baada ya barabara kuu kutopitika kutokana na mafuriko makubwa.
Kamanda Seda alionya kwamba idadi ya vifo inaweza kuongezeka huku shughuli za utafutaji na uokoaji zikiendelea katika maeneo kadhaa yaliyoathiriwa vibaya na mafuriko.
Pia unaweza kusoma: