Wanajeshi wa Marekani waliuuawa katika mzozo wa Iran watambuliwa
Jeshi la Marekani limewataja wanajeshi wake wa kwanza kuuawa katika mzozo kati ya Marekani na Iran.
Wanajeshi sita walikufa wakati "mfumo wa ndege isio na rubani" ulipokwepa ulinzi wa anga na kugonga kituo cha amri katika bandari ya Shuaiba, nchini Kuwait, Jumapili.
Kamandi Kuu ya Marekani hapo awali ilisema wanajeshi watatu walifariki katika shambulio hilo, lakini maafisa walithibitisha Jumatatu kwamba idadi ya waliofariki iliongezeka maradufu, baada ya mtu mmoja kufariki dunia kutokana na majeraha na miili miwili zaidi kupatikana kwenye vifusi.
Wanajeshi hao wa Akiba wa Jeshi la Marekani ni wa Kamandi ya 103 ya Ulinzi ya Des Moines, Iowa, ambao ni:
- Kapteni Cody A. Khork, 35, wa Winter Haven, Florida
- Sajenti Daraja la kwanza Noah L. Tietjens, 42, wa Bellevue, Nebraska
- Sajenti wa Daraja la kwanza Nicole M. Amor, 39, wa White Bear Lake, Minnesota
- Sajenti Declan J. Coady, 20, wa West Des Moines, Iowa
Siku ya Jumatatu Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth alisema kwamba ngome ya kijeshi ya Marekani huko Kuwait ilipigwa wakati shambulio la kulipiza kisasi lililofanywa na Iran.
Vifo hivyo sita pekee ndivyo vilivyothibitishwa na jeshi la Marekani tangu lilipoanzisha mashambulizi dhidi ya Iran kwa ushikiano na Israel.
Unaweza kusoma: